• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

NAIBU KATIBU MMUYA AIPONGEZA MOROGORO KWA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE.

Posted on: April 22nd, 2022


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Kaspar Mmuya ameipongeza Serikali Mkoani Morogoro kwa usimamizi vema utekelezaji wa Afua ya Lishe kati ya Serikali na Sekta binafsi ili kudhibiti udumavu, ukondefu, na ukosefu wa Madini muhimu mwilini kupitia chakula katika jamii.

Naibu Katibu Mkuu huyo ametoa pongezi hizo Aprili 21 Mwaka huu katika ziara ya kikazi ya siku mbili aliyoifanya Mkoani Morogoro na kutembelea wadau mbalimbali wanaohusika na utekelezaji wa Afua ya lishe ili kujiridhisha namna ya utekelezaji wake, ambapo alitembelea Viwanda vidogo kadhaa vinavyojihusisha na urutubishaji wa virutubisho katika unga wa sembe ambao ni chakula kikuu kwa jamii ya Watanzania walio wengi.

Naibu Mmuya amesema Mkoa wa Morogoro Umepiga hatua kubwa kwani kwa takwimu za Mwaka 2018 ulikuwa nafasi ya 25 kitaifa katika utekelezaji wa Afua za lishe ambapo kwa takwimu za mwaka huu 2022 Mkoa huo umeshika nafasi tano bora Kitaifa katika utekelezaji wa Mradi wa Afua za Lishe.

Katika hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu huyo amemuagiza Afisa Biashara wa Mkoa huo kuwatembelea wamiliki wa Mashine za unyunyiziaji wa virutubishi katika unga wa sembe ili kujua na kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wamiliki hao katika utendaji kazi wao hususan changamoto za mitaji ya kuendeshea shughuli zake.

Katika ziara hiyo, Naibu Katibu Mkuu Mmuya amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameshaagiza kuwepo kwa ushirikiano baina ya Sekta za Umma na Sekta Binafsi kufanya kazi kama timu katika utekelezaji wa afua za lishe ili kufikia malengo ya mpango wa pili wa utekelezaji wa afua za lishe ulioanza Mwaka huu hadi Mwaka wa 2025, ambao unalenga kutimia kwa lishe bora kwa Watanzania wote kwa asilimia mia moja.

Kwa upande wake Meneja wa Kampuni ya SANKU inayojihusisha na kuwasaidia wazalishaji wa kati na wa wadogo katika uwekaji wa virutubishi kwenye vyakula Bw. Omary Gwau amesema kazi yao ni kuisaidia Serikali kupambana na udumavu hapa nchini na kwamba hadi sasa wameshazifikia Wilaya 102 na wazalishaji zaidi ya 700, ambapo Mkoa wa Morogoro pekee wazalishaji 115 wamefikiwa na kuufanya Mkoa huo kushika nafasi ya pili Kitaifa nyuma ya Mkoa wa dar es salaam ambao zaidi wa wadau 120 wamefiwa.  


Aidha, Mkurugenzi wa huduma ya urutubishaji wa virutubisho kutoka Wizara ya Afya Bw. Celestine Mgoba amesema katika kuhakikisha wananchi wanapata lishe bora nje ya kurutubisha unga wa sembe, pia wanafanya urutubishaji kwa kuweka virutubishi katika chumvi, ngano na mafuta ya kula inayopelekea kupungua kwa udumavu, kuongeza uzito na ukosefu wa madini muhimu kwa zaidi ya asilimia 1.8 nchini kote.


Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TBS amesema wana jukumu kubwa la kusimamia uwekaji sahihi wa virutubishi katika bidha husika ili wananchi waweze kupata bidhaa bora na kuwezesha mlo kamili ambao utapelekea upatikanaji wa lishe bora na kuwezesha malengo ya Serikali ya Mpango ya Afua za lishe kufikiwa kikamilifu ifikapo Mwaka 2025.



Akiwakilisha wadau wa utekelezaji wa uwekaji wa virutubisho katika vyakula ikiwemo unga wa mahindi, Bw. Dornath Makata ambaye ni mmiliki wa kampuni ya uzalishaji ya ASANTE MUNGU iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro amebainisha changamoto zinazowakabili katika utekelezaji wa program hiyo ambapo amesema changamoto kubwa ni ukosefu wa elimu kwa walaji na ukosefu wa mitaji kwa watekelezaji wa uwekaji wa virutubishi katika vyakula.



 

MWISHO.

























































Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.