• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

NAIBU WAZIRI MKUU ATAKA MAELEZO KWA WAAJIRI WASIOTUMA WASHIRIKI - SHIMIWI

Posted on: September 25th, 2024

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko (MB) amewataka Waajiri na Wakuu wa Taasisi za umma hapa nchini ambao hawakupeleka watumishi wao kushiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kutoa maelezo ya sababu zilizowafanya kutowaruhusu watumishi hao kushiriki michezo hiyo.

Mhe. Dkt. Biteko ametoa agizo hilo Septemba 25, Mwaka huu wakati akifungua rasmi  mashindano ya SHIMIWI yanayofanyika katika viwanja mbalimbali vya michezo vilivyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo.

Amesema, kama suala hilo halitekelezeki au lina changamoto basi ni vema jambo hilo  likaondolewa au likaboreshwa, lakini kwa sasa kwa kuwa tayari serikali ilishatoa ruksa na kufanya makubaliano ya pamoja, jambo hilo sio la hiari tena bali ni lazima.

Kwa sababu hiyo, Mhe. Doto amemwagiza Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na utawala bora kutoa maelekezo kwa waajiri na wakuu wa Taasisi wote kuendelea kutenga bajeti ya michezo ya SHIMIWI pamoja na kutoa ruhusa kwa watumishi wao bila kuwa na kisingizio chochote.

“...Kama tumekubaliana kufanya jambo lazima tulifanye, linakuwa ni lazima siyo hiari, Kama kuna sababu ya kuliboresha tuboreshe kwa kufanya mabadiliko na siyo kukubaliana bila kufanya utekelezaji...” ameagiza Mhe. Dkt. Doto Biteko.

Dkt. Biteko amechukua hatua hiyo kutokana na kushuka kwa idadi ya vilabu vinavyoshiriki mashindano hayo kutoka 74 mwaka 2023 hadi 66 mwaka 2024 jambo ambalo amesema linaashiria uwepo wa changamoto katika uendeshaji wa michezo ya SHIMIWI.

Sambamba na hayo, Mhe. Doto Biteko amewataka viongozi wa mashindano ya SHIMIWI kuhakikisha mashindano yajayo wanaweka mpango wa kuendeleza vipaji vya watu wenye mahitaji maalum na kuyaboresha zaidi kwa ustawi wa jamii.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amepongeza juhudi za viongozi wa SHIMIWI kwa kutumia muda mchache kuandaa michezo mbalimbali kwa watumishi ili kuwa na afya ya akili na ya mwili hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wawapo ofisini.

Pia amesema, Taifa limekuwa na mwendelezo mzuri katika mashindano ya kimataifa kwani katika timu ya Taifa Stars ina nafasi nzuri kufuzu katika kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) yatakayofanyika mwakani Nchini Moroco.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Mkoa huo unasifika kuwa ni Mkoa wa kimichezo kutokana na Amani iliyopo ambayo ndio chachu ya maendeleo huku akiwahakikishia wanamichezo waliofika mkoani humo kufanya michezo yao kwa utulivu na amani.

Hata hivyo, Mhe. Malima amewataka wanamichezo hao mara baada ya kuhitimisha michezo hiyo watumie fursa hiyo kutembelea vivutio vya utalii vinavyopatikana Mkoani Morogoro vikiwemo Mbuga ya wanyama ya Mikumi, hifadhi ya Mwalimu Nyerere na milima ya Udzungwa yenye vivutio vya kila aina yakiwemo maporomoko ya maji.


Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.