• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

NAIBU WAZIRI WA MICHEZO NA UTAMADUNI AYASHAURI MAJESHI.

Posted on: September 15th, 2024


Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amelishauri Baraza la Michezo ya Majeshi Tanzania (BAMMATA) kuendeleza michezo mbalimbali katika makambi ya majeshi na sehemu za kazi ili kuibua vipaji vipya lakini bila kusahau kutekeleza jukumu lao la msingi la Ulinzi na Usalama.

Naibu Waziri Mwinjuma ametoa ushauri huo Septemba 15, 2024 wakati akifunga mashindano ya majeshi Tanzania yaliyozinduliwa Septemba 6, 2024 ambapo kwa mwaka huu mashindano hayo yamefanyika Mkoani Morogoro yakiwa na kaulimbiu inayosema "michezo ni furaha, Afya na ajira".

Amesema, kuna umuhimu mkubwa wa wanamichezo kutoka jeshini kushiriki michezo mbalimbali na kuweza kuliwakilisha Taifa katika mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa hivyo ni jukumu lao kuweka mazingira wezeshi kwa wanamichezo hao ili kuweza kufikia malengo.

"..Juhudi za kuendeleza michezo katika makambi na sehemu za kazi zizidi kuimarishwa na kuendelezwa.."  Amesema Hamis Mwinjuma

kiongozi huyo ameendelea kutoa ushauri kwa Baraza hilo kuendelea kushirikiana na Wizara yenye dhamana ya michezo na mashirikisho ya vyama vya michezo nchini katika kuweka taratibu ambazo zitawezesha majeshi yetu kuendelea kutoa wawakilishi wengi wanaoliwakilisha Taifa katika mashindano ya Kimataifa.

Sanjari na hayo amelishauri Baraza hilo kuendelea kutoa  mafunzo kwa walimu na waamuzi, kujenga viwanja vya michezo, na kuendeleza programu za kukuza na kuendeleza vipaji kwa vijana katika michezo ili kutengeneza wanamichezo watakaoshiriki mashindano mbalimbali.

Aidha, Naibu Waziri ameyataka majeshi yote kuendelea kutekeleza jukumu lao la msingi la kulinda watu na mali zao ili kuimarisha ulinzi na Usalama hapa nchini na taifa kuendelea kubaki kuwa kisiwa cha AMANI.

"Jambo la muhim kabisa, nichukue fursa hii kuwakumbusha  utekelezaji wa jukumu lenu la msingi ambalo ni Ulinzi wa taifa letu na mipaka yake...." amesisitiza Naibu Waziri.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema michezo hiyo katika mkoa huo imefanikiwa kwa kiwango kikubwa na wanamichezo wameonesha vipaji vyao huku akilishauri BAMMATA mwakani tena kuleta mashindano hayo mkoani Morogoro.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Michezo ya Majeshi Tanzania (BAMMATA) Brigedia Jeneral Saidi Hamisi  Saidi ameishukuru Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Baraza la Michezo Taifa (BMT) kwa kuwezesha kutoa msaada wa kiufundi kwa BAMMATA huku akisema kumalizika kwa mashindano hayo ni muda wa kwenda kujipanga kwa ajili ya kushiriki mashindano ya kitaifa na kimaifa.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.