• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

NeST MWAROBAINI WA KUPUNGUZA MILOLONGO YA MANUNUZI YA UMMA SERIKALINI

Posted on: August 29th, 2023

Mikoa yote hapa nchini kwa sasa ipo katika harakati za utoaji wa mafunzo ya mfumo mpya wa kielektroniki wa manunuzi ya Umma unaojulikana kama National e – Procurement system (NeST).

Mfumo wa NeST ni mbadala wa mfumo wa manunuzi ya Umma unaotumika sasa unaojulikana kama Tanzania National e Procurement System (TANePS) ulioanzishwa takribani miaka minne iliyopita.

Mfumo huu wa NeST ambao unaelezwa kuwa ni mfumo ulioundwa na wataalam wazawa wa Tanzania unaokuja kuwa mwarobaini wa kutatua changamoto kubwa ya uwepo wa milolongo mingi na iliyokuwa inachukua muda mrefu wakati wa manunuzi ya Umma hususani  zabuni.

Changamoto hii ilitokana na mfumo wa TANePS ambao kwa namna moja au nyingine ulitoa mwanya kwa wadau wasio wazalendo wa utoaji na upokeaji wa rushwa, zabuni kutolewa kwa kufahamiana au kuwepo kwa upendeleo wakati wa michakato, hivyo kupelekea kuchelewesha mchakato wa manunuzi pamoja na gharama za bidhaa husika kuwa kubwa zaidi kuliko iliyoko sokoni.

washiriki wa mafunzo ya mfumo mpya wa kielektroniki wa Manunuzi ya umma -  National e - Procurement System (NeST) kutoka Halmashauri ya Ifakara wakiwa katika ukumbi wa mafunzo wakipewa mafunzo hayo.  nyuma kabisa ni Mkufunzi wa mafunzo hayo Bw. Leopold Ngirwa akitoa usaidizi wa kitaalamu

Faida ya mfumo wa NeST ukiachia mbali kuundwa na wazawa wa ndani ya nchi yetu na kupelekea kuwepo kwa usiri na usalama wa nyaraka zetu za hapa nchini ukilinganisha na TANePS uliokuwa unamilikiwa na wageni, mfumo huo utaongeza uwajibikaji ndani ya mfumo na kutoa wigo mpana wa wadau katika kushiriki katika ununuzi, hapa ni pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo.

Faida nyingine ni pamoja na kuharakisha michakato ya manunuzi na kupunguza matumizi ya nyaraka kwa kuwa na kazi kubwa za manunuzi zitazokuwa zinafanyika ndani ya mfumo na sio  nje ya mfumo wa NeST, hivyo kuongeza thamani ya fedha yaani value for money kwa bidhaa husika.

Mafunzo hayo kwa sasa yanatolewa kwa ngazi ya Halmashauri kwa wataalamu sita (6) kutoka kila Halmashauri wakiwemo Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA, Vitengo vya Manunuzi, Wakaguzi wa Ndani, Maafisa Mipango wa Halmashauri na wahasibu wa Halmashauri.

Awali, mafunzo ya mfumo wa NeST yalitolewa Jijini Dodoma kwa Wataalamu sita (6) wa kutoka kila Mkoa yaliyofanyika kuanzia Julai 31 hadi Agosti 4 mwaka huu ambayo yaliendeshwa chini ya Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) wakishirikiana na Wataalamu mbalimbali kutoka PPRA na wakufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma.

Mimi kama Mtanzani,  nichukue fursa hii kuipongeza sana Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma hapa nchini (PPRA) kwa kuliona hilo na kubuni mbinu mpya ya kudhibiti fedha za Serikali ambazo ni kodi za wananchi zilizokuwa zinavuja kupitia eneo hili la manunuzi.

 

Sambamba na pongezi hizo kwa Serikali, kwa mujibu wa maelezo yanayotolewa kupitia mafunzo hayo ni kwamba mfumo wa TANePS utazimwa ifikapo mwezi Septemba mwaka huu na mfumo wa NeST utaanza kutumika rasmi kuanzia mwenzi Oktoba mosi mwaka huku kukiwa na angalizo kuwa taasisi yoyote itakayofanya manunuzi nje ya mfumo wa NeST baada ya mwezi Oktoba basi wahusika wake watachululiwa hatua kali za kinidhamu.

 

Wadau wanaunga mkono hatua hiyo ya Serikali na kwamba isisite kamwe kutekeleza maagizo yake ya kumchukulia hatua mkuu yoyote wa Taasisi ambaye hatatumia mfumo wa NeST, kwa kuwa kufanya hivyo Serikali itaokoa fedha nyingi zilizokuwa zinateketea bila sababu za msingi lakini pia kwa kutumia mfumo huu mpya itatoa fursa kwa wazabuni kupatikana kihalali.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.