• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

NSSF MOROGORO YAPONGEZWA KWA KUZIFIKIA SEKTA ZISIZO RASMI MKOANI HUMO.

Posted on: December 16th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa ameupongeza Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoani Morogoro kwa kupanua wigo wa utoaji huduma hapa nchini kwa kuwafikia wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga, wachimbaji wadogo na wasanii katika Mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akiongea na Viongozi, Waajiri, wafanyakazi na wanachama wa mfuko wa NSSF Morogoro kwenye ufunguzi wa kongamano la waajiri Mkoani Morogoro.

Mhe. Fatma Mwassa ametoa pongezi hizo Disemba 16 mwaka huu wakati akifungua kongamano la Waajiri katika Mkoa wa Morogoro lililowakutanisha waajiri kutoka Mashirika, na Taasisi mbalimbali katika Mkoa huo.

kongamano hilo limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa NSSF uliopo katika Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Fatma Mwassa akipokea zawadi kutoka kwa viongozi wa mfuko wa NSSF baada ya ufunguzi wa kongamano la waajiri Mkoani Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema NSSF katika Mkoa huo imehakikisha kuwa waajiri wanatekeleza wajibu wao wa msingi wa kuwasilisha michango ya waajiriwa wao kwa wakati hivyo kuepusha migogoro na waajiriwa wao.

“... NSSF imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha waajiri wanatekeleza jukumu lao la msingi la kuwasilisha michango kwa wakati lakini pia ninaziona juhudi kubwa za NSSF Morogoro katika kuhakikisha makundi mbalimbali ya sekta isiyorasmi yanaandikishwa, hongereni sana wananssf Morogoro kwa kazi nzuri..” amesema Mhe. Fatma Mwassa.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kwa sasa watanzania wanaziona juhudi za shirika hilo kwa sababu sehemu kubwa ya makusanyo ya fedha zinatumika kutekeleza miradi mikubwa ambayo inaikuza NSSF kama shirika na watanzania wote.

Sambamba na hilo, Mhe. Fatma mwassa ametumia kongamano hilo kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kusimamia sekta ya hifadhi za jamii hapa nchini, na kuridhia kanuni mpya ya kikokotoo ambacho kimenufaisha kundi kubwa la wananchama wa NSSF.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewasisitiza waajiri katika Mkoa huo kuendelea kutekeleza wajibu wao wa msingi wa kuwaandikisha wafanyakazi wao katika mfuko wa NSSF pamoja na kuwasilisha michango yao stahiki kwa wakati.

Awali Meneja wa NSSF Mkoa wa Morogoro Bi. Amina Kassim wakati akitoa tathimini ya utendaji wa kazi wa NSSF katika Mkoa huo amesema kazi kubwa ya NSSF Morogoro ni kuwaandikisha waajiri na wanachama, kukusanya michango, kuwekeza na kulipa mafao kwa wanachama wake.

Meneja wa Mfuko wa NSSF Mkoani Morogoro Bi. Amina Kassim akitoa tathmini ya utendaji wa NSSF Morogoro kwenye ufunguzi wa Kongamano la waajiri Mkoa wa Morogoro.

Amesema NSSF Morogoro inakusanya kiasi cha shilingi Bilioni sita kwa mwezi na kulipa mafao Bilioni Moja nukta Moja kwa mwezi, ameongeza kuwa Mfuko huo unawanachama 338,000 na wastaafu hadi kufikia mwezi Novemba mwaka huu 2022 walikuwa 1,269.

Aidha, Bi. Amina Kassim ametaja miradi ambayo NSSF katika Mkoa huo inamiliki ikiwemo Mradi wa Kiwanda cha Sukari cha Mkurazi kilichopo Wilayani Kilosa, ambapo kinatarajia kuanza uzalishaji mwezi Machi 2023, pia inajengo la Mafao ambalo ni kitega uchumi cha NSSF pamoja na ofisi za kupangisha ambazo baadhi ya taasisi za kibenki zimekodi.

Pamoja na mafanikio hayo Meneja huyo amesema kunachangamoto ambazo wanakutana nazo zikwemo za waajiri kuchelewa kupeleka taarifa za wanachama wao kwa wakati, waajiri kutowasajiri wafanyakazi wao katika Mfuko, waajiri kushindwa kutoa mikataba kwa wafanyakazi wao.

Kwa upande wake Bw. James Oigo Meneja Usimamizi wa Mafao kutoka Makao makuu ya NSSF amesema kupitia makongamano hayo yanawezesha kuwafikia wafanyakazi wengi zaidi, na lengo la makongamano hayo ni kutoa elimu, kukumbushana wajibu wa wanachama na waajiri pamoja na kupokea mrejesho kutoka kwa wanachama wao.

Meneja Usimamizi wa Mafao ya Mfuko wa NSSF Bw. James Oigo akiongea na waajiri, viongozi na wanachama wa mfuko huo.

Kongamano hilo lina lengo la kutoa elimu ya hifadhi za jamii kwa waajiri, kutoa elimu ya mabadiliko ya kisheria ya hifadhi za jamii kama ile ya kikokotoo, kuwakumbusha waajiri kupeleka michango ya wafanyakazi katika mfuko, na kutoa elimu ya matumizi ya Tehama katika kukusanya na kuhifadhi taarifa za waajiri na wafanyakazi katika mfumo wa kielektroniki.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akitoa zawadi kwa waajiri wa Mkoa wa Morogoro kwa kutekeleza wajibu wao wa kisheria katika mfuko huo wa NSSF.

Baadhi ya picha za Mhe. Fatma Mwassa akiwa kwenye picha pamoja na waajiri, viongozi, wafanyakazi na wanachama wa NSSF Mkoa wa Morogoro baada ya ufunguzi wa kongamano la waajiri Mkoani humo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.