• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

OCD, OCCID WASIMAMISHWA KAZI.

Posted on: February 21st, 2023

Kutokana na malalamiko ya wananchi juu ya jeshi la polisi Wilayani Kilombero kutotimiza wajibu wao wa kulinda raia na mali zao, Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Mhe. Hamad Masauni amewasimamisha kazi Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kilombero (OCD) Shedrack Kigobanya pamoja na Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai wa Wilaya hiyo Daudi Mshana ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizotolewa dhidi yao.

Waziri Masauni amechukua uamuzi huo Februari 20 mwaka huu wakati wa hotuba yake mbele ya wananchi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani vilivyoko katika Mji mdogo wa Ifakara Mkoani Morogoro.

Mhe. Masauni amesema amegundua uwepo wa mapungufu mengi ambayo yamepelekea wananchi kuwa na kero nyingi dhidi ya OCD Huyo na kuwaasababishia matatizo mengi, sababu kuu ni kushindwa kusimamia vema kazi yake ya kuhakikisha kuwa jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo inatekeleza majukumu yake ipasavyo.

“...nataka niwaambieni Serikali yenu ya awamu ya sita haitakubali kuona mwananchi yoyote anaonewa... na ndio maana tunamsimamisha kazi mara moja OCD wa hapa ameshindwa kusimamia kazi yake vizuri ya jeshi la Polisi katika Wilaya hii...."amesema Waziri Masauni.

Aidha, Mhe. Masauni ameliagiza Jeshi la Polisi hapa nchini kuhakikisha kuwa linaimarisha mifumo ya utendaji kazi kuanzia ngazi ya kata hadi Mkoa, wakati huo huo Waziri huyo amewataka wananchi kuimarisha ushirikiano baina yao na Jeshi la polisi ili kufichua viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani.

Moja ya kero kubwa zilizotajwa na wananchi ni Askari wa jeshi hilo kuwanyanyasa wananchi, kutofanyia kazi malalamiko kwa wakati  pamoja na kuwanyang'anya mali  wananchi hao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Ifakara Mhe. Kassim Nakapala ameipongeza na kuishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wake na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya hiyo.

Nae, Bwana Boniface Mmanga mkazi wa Ifakara amesema Jeshi la Polisi ndiyo tegemezi katika kulinda usalama wa raia na mali zao hapa nchini lakini, polisi katika Wilaya ya Kilombero wamekuwa kero kubwa kwa wananchi hali ambayo imewafanya kukosa imani kwa jeshi hilo na kumuomba Waziri huyo wa kuwapatia ufumbuzi juu ya kero zao zinazosababishwa na jeshi  la Polisi.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.