• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

PROGRAM YA URASIMISHAJI WA UJUZI WA WAFUNGWA NJE YA MFUMO RASMI YAZINDULIWA MOROGORO.

Posted on: March 11th, 2025



Programu ya urasimishaji wa ujuzi nje ya mfumo rasmi imezinduliwa kwa mara ya kwanza Mkoani Morogoro katika Gereza la Mtego wa Simba, ambapo wafungwa 201 wamehitimu mafunzo mbalimbali ya ufundi, ukiwemo ujenzi na kutunukiwa vyeti vya ujuzi huo.

Uzinduzi huo umefanyika Machi 11, 2025, ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Innocent Bashungwa, katika Gereza la Mtego wa Simba, lengo likiwa ni kurasimisha ujuzi wa wafungwa hao ili kubadilisha mienendo na tabia zao watakapotoka gerezani kuweza kujitegemea na kuwa tegemeo kwa jamii na taifa.

Akifafanua zaidi, Waziri Bashungwa amesema historia kubwa imeandikwa, kwani programu hiyo itawasaidia wafungwa na kusisitiza kuwa wafungwa watakaokuwa wamepata mafunzo hayo wakiwa gerezani na kupata vyeti watanufaika na mikopo ya asilimia 10, pamoja na kuwa na mfuko maalum wa kuwawezesha kujipatia mitaji pale watakapomaliza muda wao gerezani.

Sambamba na hayo, Waziri huyo amewaasa wafungwa waliopo magerezani kujifunza kwa bidii na kurekebisha tabia zao, kwani jamii inawategemea na inajengwa na wao katika misingi ya maadili mema kwa manufaa ya taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amelitaka Jeshi la Magereza kutumia rasilimali walizonazo kama misitu na mashamba kuwafundisha wafungwa ujuzi wa kilimo, ili wanapomaliza vifungo vyao waweze kutumia maarifa hayo kufanya mapinduzi ya kilimo na kukuza vipato vyao na uchumi wa taifa.

Kwa mujibu wa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania CGP Jeremiah Katungu amesema mafunzo hayo yanajumuisha ufugaji, ujenzi, utengenezaji wa samani, ususi na elimu katika ngazi zote, kuanzia msingi hadi chuo.

Jitihada hizo zimekusudiwa kuwawezesha wafungwa kuwa raia wema na wenye uwezo wa kujitegemea wanapomaliza vifungo vyao magerezani.


Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.