• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aitaka JMAT Kupinga Ukatili.

Posted on: January 24th, 2025



Rais mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, ameitaka Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika juhudi za kupinga ukatili hapa nchini.

Mhe. Kikwete amesema hayo Januari 23, mwaka huu wakati akifungua kikao cha kamati kuu cha JMAT kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Morena iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akifafanua zaidi, Mhe. Jakaya Kikwete amesema ukatili huo hususan kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) ni changamoto inayohitaji mshikamano wa kijamii na elimu ya kina ili kuutokomeza kupitia kampeni za kitaifa, huku akibainisha kuwa JMAT inao uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko kwa kuunganisha nguvu za viongozi wa kidini, vyombo vya habari na wananchi wenyewe.

"Tunahitaji kuhakikisha kuwa imani potofu na vitendo vya kikatili vinakemewa kwa nguvu zote ili kudumisha heshima ya kila binadamu." Amesema Mhe. Jakaya Kikwete

Sambamba na hayo, Rais huyo mstaafu ameipongeza JMAT kwa kazi kubwa ya kuimarisha amani na mshikamano wa Taifa na kuwahimiza kuendelea kufanikisha malengo yao kwa kushirikiana na Serikali na taasisi nyingine ili kuhakikisha kuwa haki, usalama na utu wa kila Mtanzania vinaheshimiwa bila kujali tofauti zao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima kwa niaba ya Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Peter Pinda ambaye ndiye mlezi wa JMAT Taifa, amewapongeza JMAT kwa kuendeleza na kudumisha falsafa ya 4R za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye anahimiza masuala ya maridhiano, ustawi wa kijamii, maendeleo ya rasilimali watu, na utunzaji wa mazingira.

Hata hivyo, Mhe. Adam Malima ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa huo kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za kiuchumi pamoja na ushiriki katika ujenzi wa miradi ya maendeleo kwa lengo la kuimarisha ustawi wa jamii na kukuza uchumi wa taifa.

Awali, Mwenyekiti wa JMAT Taifa, Alhaji Dkt. Mussa Salim, amesema kuwa JMAT si chombo cha kidini bali ni Jumuiya inayosimamiwa na viongozi wa dini, kwani kila mtu ana dini yake kwani baadhi ya Watanzania wana dhana potofu kwamba Jumuiya hiyo inalenga kuanzisha dini mseto, jambo ambalo si sahihi.

Pia, Dkt. Salim amebainisha kuwa Watanzania wote ni ndugu, na udugu huo unapaswa kuunganisha na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za maendeleo zikiwemo  ujenzi wa miradi kama zahanati, misikiti, makanisa, uchangiaji wa damu salama, kutembelea watoto yatima na kuiombea serikali ili iendelee kutunza na kudumisha amani hapa nchini.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.