• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AAGIZA WAVAMIZI WA VYANZO VYA MAJI KUONDOLEWA.

Posted on: November 1st, 2022

Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewaagiza Wakuu wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam pamoja na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Dar es salaam (DAWASA) kufanya ukaguzi na kuwaondoa wavamizi wote wa vyanzo vya maji ili kuongeza upatikanaji wa uhakika wa maji katika Mikoa hiyo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wananchi na viongozi waliohudhuria kwenye Mjadala wa Kitaifa wa Nishati Safi ya kupikia katika ukumbi wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo Novemba 1 mwaka huu wakati akifungua Mjadala wa kitaifa wa Nishati safi ya kupikia ambapo kitaifa unafanyika katika ukumbi wa mikutano wa J.K. Nyerere jijini Dar es salaam.

Akifafanua zaidi Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema upungufu wa maji katika mto Ruvu unachangiwa na ukame unaotokana na shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji kama vile ukataji wa misitu kwa ajili ya kilimo na kuni, kilimo cha umwagiliaji, ufugaji wa samaki katika mabwawa shughuli ambazo kwa kiasi fulani zimesababisha baadhi ya mito kukauka.

“...sasa Mkuu wa Mkoa Dar es salaam na Pwani, lakini pia na DAWASA nataka muhakikishe kwamba mmekwenda na mmmehakikisha zile ‘blocks’ zote zilizopo kwenye mito zimeondoka...” amesema Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wao Wadau wa Sekta ya Nishati Mkoani Morogoro wameshauri uimarishaji wa utunzaji wa vyanzo vya maji ili kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa maji na kupata nishati safi ya kupikia kupitia umeme wa maji hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa (wa nne kutoka kulia) akiwa pamoja na  viongozi wengine wa Mkoa na Wilaya wakishiriki Mjadala wa kitaifa wa Nishati safi ya kupikia katika ukumbi wa mikutano Hoteli ya Morena, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akitoa ushauri huo Mhandisi Jane Kadoda kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi  wa Mazingira Tanzania (NEMC) Kanda ya Morogoro-Rufiji amesisitiza watanzania kutunza vyanzo vya maji ili kuongeza kiwango cha maji katika bwawa la Mwalimu Nyerere na hivyo nishati safi ya kupikia kupitia umeme ipatikane na iwe endelevu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amesema kuna haja ya kusimamia sheria zilizopo sasa au kuziongezea makali katika kulinda mazingira, kutokana na uwepo wa shughuli nyingi za kibinadamu zinazoharibu mazingira ikiwemo uchomaji wa mkaa na ufugaji mifugo mingi kupita kiasi.

Sambamba na hayo Mkuu huyo wa Mkoa ameshauri kamati itakayoundwa ambayo imeagizwa na Mhe Samia Suluhu Hassan iweze kutembelea visiwa vya Pemba kwa lengo la kujifunza namna bora ya kutunza mazingira.

Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mathayo Maselle akitoa mchango wake kuhusu mijadala ya kuboresha nishati safi ya kupikia.

Mkuu wa Wilaya ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Albert Msando akichangia hoja kwenye mjadala wa kitaifa wa Nishati safi ya Kupikia.

Akichangia hoja hiyo ya mjadala wa Nishati safi ya kupikia Fatma Mwassa amefafanua kuwa Mkoa wa Morogoro utakuwa shamba la mazao ya matunda na viungo mbalimbali vikiwemo karanga miti, hiriki, mdarasini na Karafu.

Mjadala wa wadau wa nishati umelenga kujadili namna bora ya upatikanaji wa nishati safi ya kupikia isiyo na athari kwenye mazingira kama vile matumizi ya nishati ya gesi na umeme.

Mjadala huo unatarajia kuendelea Novemba 2 mwaka huu, huku mikoa ya Dodoma, Iringa, Tabora, Shinyanga na Morogoro ikishiriki mubashara kwa njia ya mtandao.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.