• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN APONGEZWA NA WANANCHI MOROGORO

Posted on: October 6th, 2022

Wakazi wa Kijiji cha Changarawe Kata ya Masanze wilayani kilosa Mkoani Morogoro wamempongeza Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajengea Kituo cha Afya kinachotarajiwa kwenda kuokoa vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi.

Bwana Jonathan Wilson Diwani Kata ya Masanze akitoa pongezi mbele ya Mkuu wa Mkoa. 

Pongezi hizo zimetolewa na wananchi wa Kijiji cha Changarawe Oktoba 5 mwaka huu wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa aliyoifanya Wilaya Kilosa kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo Wilayani humo ukiwemo mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Masanze.

Muonekano wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika kituo cha Afya Masanze Wilayani Kilosa.

 Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji hicho wamesema wamekuwa wakitembea umbali wa zaidi ya kilomita 20 kwenda kufuata huduma ya Afya Mjini Kilosa huku baadhi ya wajawazito wakipoteza maisha kutokana na kuchelewa kufika maeneo ya kutolea huduma ya Afya.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa akizungumza na wananchi wa Masanze Wilayani Kilosa

Miongoni mwa wakazi wa Kata ya Masanze akiwemo Bi. Evalina Moreli, amesema kuwa kabla ya kituo hicho kujengwa wananchi walikuwa wanatembea umbali wa zaidi ya kilometa 20 kufuata huduma ya matibabu Mjini Kilosa ambapo watoto chini ya miaka 5 na wajawazito wamekuwa wahanga wakubwa kutokana na ukosefu wa kituo cha Afya, kwa sasa wanamshukuru  Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajengea kituo hicho cha Afya.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Dkt. Mamisa Basike amesema kuwa Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha kiasi cha Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa kituo cha afya cha Masanze ambacho wanategemea kitaokoa maisha ya wajawazito na watoto kundi ambalo limekuwa na changamoto ya kuhatarisha maisha yao.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaj Majid Mwanga akitoa shukrani zake kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa akizungumza na wananchi mbele ya Kituo hicho cha Afya ameiagiza kamati ya Ujenzi ya Kituo hicho cha Afya pamoja na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kukamilisha kwa wakati ujenzi wa majengo yaliyobaki na kuhakikisha yanapata vifaa tiba ili matumizi ya majengo hayo yaanze mara moja.

“.... sasa tukamilishe majengo yote yaliyoanzishwa mpaka yafike mwisho, lakini cha pili tuweke vifaa tiba majengo yote yaliyokamilika ili matumizi yake yaanze mara moja....” amesema Fatma Mwassa.

Kufuatia changamoto za Afya zilizokuwa zikiwakabili wananchi wa Kata ya Masanze, Serikali hadi sasa imekwisha peleka fedha zilizotengwa kwa ujenzi wa kituo hicho cha Masanze ambazo ni shilingi milioni 500.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.