• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AAGIZA WANAFUNZI KULA CHAKULA SHULENI

Posted on: September 2nd, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amewaagiza watendaji wa Serikali Mkoani humo kuhakikisha wanafunzi wote wa shule za msingi na Sekondari wanakula chakula shuleni ili kujenga afya na kuongeza umakini darasani.

Dkt. Mussa ametoa agizo hilo Septemba 2, mwaka huu wakati wa mwendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kutembelea shule za Msingi na Sekondari zilizopo Mkoani humo  akitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero lengo likiwa ni kuangalia hali ya lishe mashuleni.

Akifafanua, Dkt. Mussa amesema, hadi sasa wanafunzi wanaokula chakula shuleni ni wachache badala yake wengi wananunua vyakula kwa fedha zao hali ambayo si salama kwa Afya zao huku wengine hula baada ya kurudi nyumbani kwao.

Kwa sababu hiyo, Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka Viongozi wa shule zote hususan watendaji wa Serikali kutumia mbinu mbadala kuzungumza na wazazi ili kuchangia chakula au fedha ili kuhakikisha wanafunzi kupata chakula kikiwa na mboga mboga pamoja na matunda.

"... ni lazima wanafunzi wote wale shuleni kwa njia yoyote tutakayokubaliana kati yetu na wazazi..." Ameagiza Dkt. Mussa Ali Mussa

Aidha, Dkt. Mussa amekemea vikali wanafunzi kula chakula cha aina moja hususan makande na ugali bila mboga mboga wala matunda kwani amesema chakula cha aina moja  hudumaza afya ya akili na kusababisha ufaulu kushuka darasani.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mussa ametaka kila shule kuhakikisha inalima mboga mboga na mazao ya biashara kama mishelisheli na mikarafuu ili shule hizo ziweze kujitegemea kiuendeshaji.

Kwa upande wake, Afisa lishe wa Mkoa wa Morogoro Bi. Salome Magembe ameishauri Kamati ya Shule ya msingi ya Dibamba kuwa na vyakula vya aina nyingi hususan vinavyozingatia lishe bora kama wanga, protini na vitamini ili kupata wanafunzi mahiri ambao ndio wataalamu wa Taifa la kesho.

Naye, Afisa Afya wa Mkoa wa Morogoro Bi. Prisca Laurent Gallet amewasisitiza walimu  kuhakikisha wanasimamia usafi katika maeneo yote ya shule ukiwemo usafi wa vyoo, kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, kuchemsha maji ya kunywa na kutenga vifaa vya kuhifadhia taka hali itakayosaidia hivyo kutasaidia kuepusha magonjwa ya kuambukiza.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.