• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA "JISOMESHE NA MKARAFUU" .

Posted on: March 16th, 2025



Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameendelea kuhamasisha kampeni ya "Jisomeshe na Mkarafuu" kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza na wakazi wote wa Wilayani Mvomero, ikiwa na lengo la kuwawezesha wanafunzi hao kiuchumi kupitia kilimo cha mkarafuu na kujisomesha kupitia kilimo cha zao hilo.

Akizungumza wakati wa zoezi la kugawa miche hiyo kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza wa shule za sekondari za Kipera na Homboza Machi 14, 2025 Dkt. Mussa amesema Viongozi wa Mkoa wa Morogoro wameanzisha kampeni hiyo kama mkakati wa kuwaandaa vijana kwa maisha ya baadaye kwa kuwawezesha wanafunzi hao kujiendeleza kimasomo kupitia zao hilo.

Ameongeza kuwa miche hiyo wanapewa wanafunzi hao bila malipo wakapande katika maeneo yao kwenye mashamba yao ama ya wazazi/ walezi wao na si kwenda kupanda mashamba au maeneo ya shule na kwamba kila mwanafunzi wa kidato cha kwanza atapewa miche 10 na kuwataka waitunza ili iweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

"...nyie wanafunzi wa form one, tunataka kila mwanafunzi mmoja leo hii, tumuachie miche ya mikarafuu kumi... miche hii isiwe mali ya shule mkaipande kwenu..." amesisitiza Dkt. Mussa

Kwa mujibu wa Katibu Tawala huyo, kwa sasa bei ya kilo moja ya karafuu ni shilingi 20,000/= hivyo, mche mmoja una uwezo wa kuzalisha kilo tano huku akisema kuwa kwa miche hiyo 10 itazalisha kilo 50 ambazo ni sawa na shilingi 1,000,000/=  hivyo, kupitia zao hilo wanafunzi wataweza kujigharamia masomo yao kupitia zao la mkarafuu. 

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Morogoro Dkt. Rozaria Rwegasira amesema kapeni hiyo ilizinduliwa rasmi Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, na inaendelea kutekelezwa halmashauri zote za Mkoa huo na sasa wako Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, huku akiwataka wanafunzi kuipokea kampeni hiyo ambayo itawasaidia kutimiza ndoto zao.

Naye, Mwl. Isakwisa Asesisye akimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero amemshukuru Katibu Tawala huyo kwa kuanzisha kampeni hiyo ndani ya Mkoa huo na sasa iko Mvomero Halmashauri yenye jumla ya shule za sekondari 37 ambapo kwa kuanzia kampeni hiyo imeanza kwa shule za Homboza na Kipera.

Nao Wanafunzi waliopatiwa miche hiyo wameeleza kufurahishwa na mpango huo, wakisema kuwa utapunguza changamoto za ada na mahitaji mengine kwao lakini pia kampeni hiyo itawajengea misingi ya kufanya kazi kwa bidii na kujitegemea.

Jumla ya wanafunzi 473 wa shule za Sekondari ya Kipera na Homboza  wamepatiwa jumla ya miche 4730 ya karafuu.


MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.