• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AENDELEZA MOTO WA KILIMO CHA MAZAO YA KIPAUMBELE.

Posted on: May 9th, 2024

RAS MOROGORO AENDELEZA MOTO WA KILIMO CHA MAZAO YA KIPAUMBELE.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameendelea na kasi ya kutoa ushauri wa bure kwa wananchi wa Mkoa huo kulima mazao ya kipaumbele likiwemo zao la Karafuu, kwa lengo la kuongeza kipato chao, Mkoa, Taifa Pamoja na utunzaji wa mazingira.

Dkt. Mussa amesisitiza na kutoa ushauri huo Mei 9, mwaka huu 2024, wakati wa zoezi la kugawa miche 300 ya karafuu katika kata ya Mzumbe kijiji cha Tangeni Wilayani Mvomero Mkoani humo.

Mara baada ya zoezi hilo Kiongozi huyo ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa Shughuli za Serikali Mkoani humo amewashauri wananchi pasi na kuwalazimisha, kukubali kulima zao la karafuu kwa kuwa litawainua kiuchumi na kuwaongezea kipato na kutunza mazingira yao.

 " ... Sote tuweze kukubali kupanda karafuu katika maeneo yetu na ukweli sio karafuu peke yake, sehemu inayoota karafuu otesha karafuu, sehemu inayoota michikichi otesha michikichi, sehemu inayoota kahawa otesha kahawa na sehemu inayoota parachichi otesha parachichi ...."  amesisitiza Dkt. Mussa.

Amesema, lengo la Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuhakikisha inawawezesha wananchi wake ili wabadilike na Maisha yao kuwa katika hali nzuri kwa kuongezeka kipato  chao kupitia kilimo cha zao la karafuu.

katika hatua nyingine Dkt. Mussa amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inaendelea na jitihada za kutafuta masoko kwa ajili ya kuuza mazao ya Iliki, karafuu, vanila na mdalasini  ambapo hadi sasa wameweza kupata soko la mazao ya karafuu na Iliki.

Akionesha shauku ya kuwainua wananchi wa Tangeni kiuchumi, Dkt. Mussa ameahidi kugharimia ziara ya mafunzo Kwenda baadhi ya maeneo ya Mkoa huo ambayo tayari wanalima zao hilo ili kujifunza na kuona uhalisia wa faida ya zao hilo la karafuu.

“…….Gari bure vile vile chakula mtakachokwenda kula kule bure, nyie mkubali tu Kwenda kuona wenzenu wanavyofaidika….” ameahidi Dkt. Mussa.

Akimkaribisha Katibu Tawala huyo kuongea na wananchi wa Tangeni kabla ya ugawaji wa miche hiyo, Katibu Tawala Msaidizizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali Dkt. Rozalia Rwegasira amewataka wananchi wa Tangeni na vijiji Jirani kupokea miche hiyo, kuipanda na kuitunza kwa manufaa yao na ya vizazi vijavyo.


Kwa upande wake Afisa kilimo wa Wilaya ya Mvomero Bi. Consolata Tarimo amesema hadi sasa wamekwishagawa miche 1000 ya karafuu ambapo miche 200 wamegawa katika kijiji cha Manza, miche 300 kijiji cha Tangeni na miche 500 wameigawa kwa wananchi wa kata ya Bunduki.

Aidha, Bi. Consolata amebainisha uwepo wa kitalu chenye miche 12000 ya karafuu kilichopo kata ya Mhonda  ambayo wamepanga kuigawa kwa wananchi wa kata mbalimbali, matarajio ni kwamba baada ya miaka mitano zao hilo litainua kipato cha wananchi wa Wilaya hiyo.

Nao wananchi wa Kijiji cha Tangeni akiwemo Bw. Mustafa Salum, Pamoja na kuishukuru Serikali ngazi ya Mkoa kuwapelekea zao la karafuu, bado wameomba kupewa mafunzo na Elimu ya namna ya kustawisha na kutunza miche ya zao hilo huku wakiomba mbegu kwa ajili ya kuotesha miche ili zao hilo liwe endelevu.

Ili kuondokana na changamoto ya uharibifu wa mazingira hususan ya ukataji hovyo wa miti, Mkoa wa Morogoro umekuja na njia mbadala ya kulima mazao ya Karafuu, kahawa, mchikichi, Parachihi na Kakao kama njia ya kutunza mazingira lakini pia kuongeza kipato kwa wananchi.

 

MWISHO. 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.