• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AHIMIZA USHIRIKIANO KWA WATENDAJI WA SERIKALI KATIKA USALAMA WA MTOTO MTANDAONI.

Posted on: March 14th, 2025


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Mussa Ali Mussa, ametoa wito kwa watendaji wa Serikali kushirikiana pamoja ili kuhakikisha mafanikio ya programu ya usalama wa mtoto mtandaoni yanafikiwa.

Dkt. Mussa ametoa kauli hiyo Machi 14, 2025, wakati akifungua mafunzo kuhusu usalama wa mtoto mtandaoni, yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Dkt. Mussa amesema Serikali imeanzisha programu mbalimbali za kusaidia wananchi, lakini utekelezaji wake umekuwa na changamoto kutokana na ukosefu wa ushirikiano miongoni mwa watendaji wa Serikali.

"Kila mmoja anafanya kazi kivyake, kila mmoja anaona kwamba hili linamwenyewe, sio la kwangu, naomba mshirikiane" alisema Dkt. Mussa.

Kwa upande wake, Mtaalamu wa Usalama Mtandaoni na Uchunguzi wa Makosa ya Kidigitali, Bw. Yusuph Kileo, amesema asilimia 87 ya mitandao ya kijamii inachangia mmomonyoko wa maadili ndani ya jamii. Amesisitiza kuwa Serikali imechukua hatua madhubuti za kulinda watoto dhidi ya ukatili na changamoto za kiusalama mtandaoni kupitia programu hiyo mpya.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bi. Mwelinde Katto, amefafanua kuwa tafiti zinaonyesha asilimia 67 ya watoto wenye umri wa miaka 12 hadi 17 wanatumia mitandao ya kijamii, huku asilimia 4 wakikutana na wahalifu mtandaoni na asilimia 5 wakilazimishwa kutuma picha za utupu.

Bi. Mwelinde ameeleza kuwa kampeni hiyo inalenga kutoa elimu kwa watoto, wazazi, walimu, na jamii kwa ujumla kuhusu usalama wa mtoto mtandaoni. Mafunzo hayo yanatolewa kwa wataalamu wa Maendeleo ya Jamii, Maafisa Ustawi wa Jamii, Wakuu wa Dawati la Jinsia la Polisi, na mashirika yasiyo ya kiserikali kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Pwani, na Dodoma.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.