• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AISHAURI TBA, AWATAKA KUFANYA KAZI KWA UFANISI

Posted on: March 21st, 2023

Katibu Tawala wa MKoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ally Mussa ameishauri Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kufanya kazi zao kwa Ufanisi, ubora na kumaliza kazi hizo ili kuondoa wasiwasi uliokuwepo kuhusu utendaji kazi wao na kwa kufanya hivyo watatoa Imani kwa Serikali na wadau wengine katika kusimamia ujenzi wa majengo.

Dkt. Mussa Ally Mussa ametoa kauli hiyo leo Machi 20, 2023 Ofisini kwake wakati akisaini Mkataba wa ujenzi wa Jengo la Ikulu Ndogo unaotarajiwa kuanza kujengwa Wilayani Malinyi.

Dkt. Mussa Ally Mussa akiwa anasini mkataba wa ujenzi 

Akifafanua zaidi mara baada ya kusaini mkataba huo, Dkt. Mussa amesema anatamani TBA ifanye kazi nzuri na kuondoa makando kando ambayo yalitaka kutokea siku za nyuma na kwamba sasa ijikite katika kufanya kazi yenye ubora, uaminifu na kuzikamilisha kazi hizo kama mkataba unavyoeleza.

“...Ofisi yangu inachokitegemea ni kwamba hii kazi inatafanyika vizuri, kwa ubora unaotakiwa.....” amesema Dkt. Mussa.

Kwa upande wake Meneja wa TBA Kanda ya Morogoro Mhandisi Rebeca Kimambo, pamoja na kutoa shukrani kwa kuiamini TBA na kupata zabuni hiyo, amemhakikishia Katibu Tawala huyo kuwa TBA itafanya kazi iliyosaini kwa ubora unaotakiwa na kukamilisha ujenzi wake kwa wakati.

“...tunaahidi kazi hii tutaifanya kwa weledi na kwa kasi ili mradi uweze kukamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa...” amesema Mhandisi Rebeca Kimambo.

Mradi huo ambao ujenzi wake unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu utakagharimu zaidi ya Shilingi Milioni 618 na unatarajiwa kukamilika mwezi machi mwaka 2024.Hadi sasa sasa Serikali imekwishatoa shilingi million 500 kwa ajili ya ujenzi huo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.