• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro akabidhi Pikipiki kwa Maafisa wa Bonde Wami Ruvu

Posted on: November 24th, 2020

RAS Morogoro akabidhi pikipiki kwa Maafisa wa Bonde, ataka zitumike kwa malengo kusudiwa

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewaagiza watendaji wa vijiji na Kata kuwa ni sehemu ya jumuiya za watumia maji zinazoendeshwa katika maeneo yao ili kulinda maslahi ya wananchi waliopo katika maeneo hayo hususan vyanzo vya maji.

Mhandisi Kalobelo ametoa agizo hilo Novemba 24 mwaka huu katika hafla fupi ya kukabidhi Pikipiki 18 kwa watumishi wa jumuiya ya Wasimamizi na Waratibu wa utunzaji wa vyanzo vya maji katika Bonde la Wami Ruvu iliyofanyika katika Ofisi za Afisa Maji Bonde la Wami Ruvu zilizoko katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mhandisi Kalabelo amesema jumuiya hizo zimeanzishwa kisheria na serikali kwa ajili ya ufuatiliaji na usimamizi wa rasilimali maji na kuhakikisha sheria zote zinazohusu maji zinalindwa kwa ajili ya kulinda vyanzo vya maji kwa maslahi ya wananchi. 

Amesema imejijitokeza hivi karibuni Maafisa wa Bonde wanapokuwa na changamoto za ukiukwaji katika kutuza vyanzo vya maji na kuzifikisha changamoto hizo kwa Watendaji wa vijiji au Kata watendaji hao wamekuwa wakiwajibu maafisa hao kuwa changamoto hizo haziko kwenye usimamizi wa Ofisi ya ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, jambo ambalo Mhandisi Kalobelo amewataka watendaji hao kuacha tabia hiyo mara moja.

“Mtendaji wa Kijiji, Mtendaji wa Kata upo pale kulinda na kuhakikisha kwamba sheria zote za Serikali zinatekelezwa, sasa nione na mniletee Mtendaji ambaye hatakuwa na kauli hiyo” alisema Mhandisi Kalobelo.

Katika hatua nyingine Mhandisi Kalobelo ametoa rai kwa wana morogoro wote kuwa wasimamizi  endelevu wa utunzaji wa vyanzo vya maji kwa sababu maisha ya kila mwanadamu yanategemea uwepo wa maji.

Aidha, amesema usimamizi wa rasilimali maji unakumbwa na changamoto mbalimbali zikiwemo shughuli za kilimo kandokando ya mito, ukosefu wa usafiri na shughuli za Kilimo hali inayopelekea upungufu wa maji ndani ya Mkoa.

Akikabidhi Piki piki hizo kwa watumishi wa jumuiya ya Wasimamizi na Waratibu wa utunzaji wa vyanzo vya maji katika Bonde la Wami Ruvu, Mhndisi Kalobelo amewataka Maafisa hao kuzitumia pikipiki hizo kwa malengo yaliyokusudiwa na yule atakayetumia pikipiki hizo tofauti na malengo (kama bodaboda) atafikishwa mahakamani na hatua za kiutumishi dhidi yake zitachukuliwa.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Morogoro – MORUWASA Julius Tanika amesema mahitaji ya maji kwa sasa katika Manispaa ya Morogoro ni Meta za ujazo 67,000 kwa siku,  ambapo kwa miaka 10 ijayo zitahitajika  Meta za ujazo 126,000 kwa siku.

Naye, Afisa maji Bonde la Wami Ruvu Simon Ngonyani amesema changamoto kubwa wanayokumbana nayo katik utendaji kazi wao wa kila siku ni uharibifu wa vyanzo vya maji hivyo kuna upungufu wa maji ukilinganisha na uhitaji wa maji kwa jamii iliyopo katika bonde la Wami Ruvu.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.