• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro aomba ushirikiano kwa watumishi

Posted on: June 3rd, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja amewataka watumishi wa Umma Mkoani humo kumpa ushirikiano wa dhati katika kutekeleza majukumu yake ili kuyafikia malengo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Serikali yake katika kufikia uchumi wa kati.

Bi. Mariam Mtunguja amesema hayo Juni  4, mwaka huu wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi kati yake na aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo  iliyofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.


Akiongea na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakuu wa Taasisi za Umma zilizopo Mkoani humo Bi. Mariam amesisitiza ushirikiano pamoja na kuheshimiana katika kufanya kazi ili kuleta tija kwa Mkoa na Taifa.

 “nawatakia kheri sana na Mwenyezi Mungu awabariki sana, lakini naomba ushirikiano mimi ni dereva tu nimekaa pale. Kama gari halina mafuta haliwezi kwenda, kama halina mataili mazuri haliwezi kwenda…” amesisitiza Bi. Mariam Mtunguja.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala huyo amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro, kila mmoja kufikisha asilimia 100 ya   makusanyo ya mapato ya ndani katika maeneo yao kabla au ifikapo Juni 30 mwaka huu.

‘’Tunaelekea tarehe 30 ya mwezi wa sita, naamimi kila Mkurugenzi amejiwekea asilimia za ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri yake, hivyo naomba mkasimamie zoezi hili kikamilifu ili tuepuke kupata hati chafu katika Mkoa wetu, Mkaguzi wa ndani hakikisha unalifuatilia hili’’ Amesema Bi. Mariam.

Kwa upande wake Mhandisi Emmanuel Kalobelo akiongea wakati wa makabidhiano hayo, amewaomba wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na watumishi wote wa Umma Mkoani humo kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Bi. Mariam Mtunguja kama ambavyo walimpa yeye ushirikiano wa kweli ili kuufikisha Mkoa huo katika malengo yaliyokusudiwa.

‘’Na nafarijika kabisa, nakabidhi mkoba katika mikono salama, sina shaka na utendaji kazi wake, ni mtu ambaye namfahamu kwa muda mrefu, nimshukuru Mhe. Rais kwa kukuchagua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro. Lakini pia niombe mtoe ushirikiano wa dhati kwake ili kuufikisha Mkoa huu tulipokusudia’’ Amesema Mhandisi Kalobelo.

 

 

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.