• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro apongeza zoezi la Anwani za Makazi, ahimiza ushirikishwaji wadau.

Posted on: October 18th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kutekeleza Mfumo wa Anwani za makazi hapa nchini na kuhimiza ushirikishwaji wa wadau mbalimbali wakiwemo Jeshi la Polisi kwa kuwa ndiyo wenye jukumu la kusimamia usalama wa raia na mali zao.


Dkt. Mussa ametoa pongezi hizo Oktoba 18 mwaka huu wakati akifungua kikao kazi cha kujadili matumizi ya mfumo wa anwani za makazi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kikao hicho kimejumuisha taasisi za umma na zisizo za umma.

Katibu Tawala huyo amesema anwani za makazi zina umuhimu katika kila nyanja ikiwemo kukuza biashara, ulinzi na usalama lakini kuna haja ya kushirikisha wadau ili kuwa na uelewa wa pamoja kutokana na umuhimu wa anwani za makazi.

“...anwani za makazi zina umuhimu mkubwa sana, kwa hiyo ombi langu katika anwani za makazi washirikisheni kwa kiwango kikubwa hawa mapolisi kwa sababu wao ndiyo wanao tulinda...” amesema Dkt. Mussa.

Aidha, Dkt. Mussa amebainisha kuwa anwani za makazi zitaisaidia serikali kukusanya mapato kutoka kwa wafanyabiashara kwa kuwa watafikika kwa urahisi katika maeneo yao.

Kwa upande wake Mratibu wa utekelezaji wa Mfumo wa Anwaniza Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Jampyon Mbugi amesema lengo la ujio wao ni kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuhakiki taarifa za anwani za makazi katika Halmashauri hiyo, na kubainisha kuwa zoezi hilo limekamilika.

Hata hivyo amesema Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro inatakiwa kutumia taarifa hizo katika utoaji wa huduma za jamii ikiwemo elimu, afya, maji, umeme na miundombinu ya barabara. Aidha, amesema Wizara inatarajia zoezi hilo kuwa endelevu katika Mkoa huo.

Naye, Mratibu wa Anwani za Makazi katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Bi. Jacqueline Mushi amesema zoezi hilo limefanyika kwa awamu tatu 2018-2019 kwa kata za Mjini, 2022 kupitia agizo la Serikali. Aidha, zoezi hilo kwa Manispaa ya Morogoro limekamilika ambapo zaidi ya asilimia 93 ya wakazi wamefikiwa kwa kata 29 za Manispaa hiyo.

Mfumo wa Anwani za Makazi ni miundombinu ambayo kwa pamoja inatambulisha mtu au kitu kilipo iwe ni ofisini, nyumbani au eneo la biashara, anwani ya makazi imeundwa na namba ya nyumba, jina la barabara na postikodi. 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.