• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO ASISITIZA USHIRIKIANO KAZINI, WANAOKWAMISHA KAZI WAWEKWE PEMBENI

Posted on: March 22nd, 2022

RAS MOROGORO ASISITIZA USHIRIKIANO KAZINI, AAGIZA WANAOKWAMISHA WAWEKWE PEMBENI

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mariam Mtunguja ametoa Wito kwa Uongozi wa Wilaya ya Gairo na Halmashauri ya Wilaya hiyo kufanya kazi kwa Ushirikiano zaidi hususani katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo huku akiagiza wanaokwamisha kazi hizo za Maendeleo kuwekwa pembeni.

Katibu Tawala ametoa maagizo hayo Machi 22 mwaka huu wakati wa ziara ya siku moja Wilayani humo alipotembelea miradi ya maendeleo ya Wilaya hiyo akiambatana na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo.



Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Mariam Mtunguja (Kulia)

Amesema,katika utendaji kazi anaamini palipo na ushirikiano na uwazi hakuna linaloshindikana na kuwataka watendaji wa Sekta ya Umma wa Halmashauri hiyo na maeneo mengine ya Mkoa huo kufanya kazi kwa uwazi na ushirikiano.

“na imani yangu mimi ni kwamba kama tukishirikiana na tukiambizana hakuna linaloshindikana” amesema Mariam Mtunguja.



RAS Morogoro (mbele aliyejifunika kilemba kichwani ) akikagua ujenzi wa majengo Hospitali ya Wilaya ya Gairo. mbele kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu Ezron Kilamhama

Aidha, amewataka Viongozi wa Wilaya na Halmashauri ya Gairo kutosita kuwaweka pembeni watendaji wa sekta ya Umma ambao wanakwamisha utendaji kazi wa wengine hususana katika utekelezaji wa Miradi ya maendeleo.

“Tukiona mtu anatukwamisha tunamuweka pembeni sisi tunaendelea,yaani hiyo msiogope kabisa, kumuweka mtu pembeni ni kitu cha kawaida kabisa katika Utendaji” amesisitiza Katibu Tawala huyo.


Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Gairo


Akiwa katika ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa barabara za mjini Gairo zilizopandishwa hadhi kutoka changarawe hadi kiwango cha lami amemtaka mkandarasi anayejenga barabara hizo kukamilisha kazi hiyo kwa wakati huku akimtaka kuanza kazi ya kuweka lami kabla ya mvua hazijaanza kunyesha.





Hata hivyo amememtaka mkandarasi wa Kampuni ya Coberg Construction Co. Limited anayepewa kazi hiyo kuhakikisha anajengea mitaro ya maji pembezoni mwa barabara hizo ili kuongeza uimara wake huku akiwataka viongozi wa Halmashauri ya Gairo kupanda miti kando ya barabara zinazojengwa ili kupendezesha Mji lakini pia mazingira yake yaweze kuendana na hadhi ya barabara hizo za Lami.



Katika Hatua nyingine Katibu Tawala huyo ametembelea ujenzi wa majengo manne yanayojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Gairo na kuagiza kuongeza mafundi wengine ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati vinginevyo fedha zake zinaweza kurudi Hazina Kuu ilhali wananchi wanahitaji huduma ya Afya.

Sambamba na hayo, amewataka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) Mkoani humo kuongeza weledi katika utendaji wao ili kuwachukulia hatua za mapema(Pro - active)  wale wote watakathubutu kujihusisha na rushwa katika miradi ya maendeleo, badala ya kusubiri mambo kuharibika na miradi hiyo kusimama hivyo kuwanyima wananchi haki yao ya kupata huduma za kijamii.







Mwisho, amewapongeza Chama na Serikali Wilayani humo kwa kufanya kazi kwa ushirikiano, na kutumia fursa hiyo kwa namna ya pekee kumshukuru Mbunge wa Jimbo hilo Ahmed Shabiby kwa kujitolea kuweka taa kwa baadhi ya Barabara za lami zinazoendelea kujenngwa Mjini Gairo na kwamba wanatambua mchango wake.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame amemhakikishia Katibu Tawala wa Mkoa kuwa yeye pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama watahakikisha wanasimamia kikamilifu miradi ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani humo  na kukamilika kabla ya Juni mwaka huu, kwani amesema kutokamilika  kipindi hicho ni tafsiri kuwa wao hawatoshi nyadhifa zao.


Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabir Makame (kushoto) akimpa maelezo RAS Morogoro juu ya ujenzi wa majengo ya Hospitali hiyo

Naye Mjumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Morogoro ambaye pia ni Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo SACP Fortunatus Musilim amesema watahakikisha wanasimamia fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya miradi hiyo zinatumika kwenye maeneo yaliyoelekezwa na si vinginevyo.



Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA)  Wilaya ya Gairo Mhandisi Masala Nkulu ameipongeza Serikali kwa kuongeza Bajeti ya TARURA mara dufu ukilinganisha na bajeti ya mwaka uliotangulia. amesema Wilaya hiyo bajeti imeongezeka kwa asilimia 250 kwa sababu hiyo amemhakikishia Katibu Tawala wa Mkoa kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.



Amebainisha kuwa TARURA kwa Wilaya ya Gairo katika Bajeti ya mwaka 2021/2022 imepangiwa na Serikali kupewa Tsh. 2,329,880,000.00 hadi sasa Serikali imekwisha toa Tsh. 1.480,165,677.19.

Katika ziara hiyo Katibu Tawala ametembelea ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, ujenzi wa Barabara ya Kichangani – Magengeni yenye urefu wa Km. 1.1  kwa kiwango cha lami ambayo hadi kukamilika kwake itagharimu Tsh.540,673,616.25 na Barabara ya Ramashop – Msingisi Guest kiwango cha lami Km.43 gharama ni Shilingi 259,326,383.75.






Miradi mingine aliyotembalea ni pamoja na Ujenzi wa Mitaro na Karavati barabara ya Ukwamani kwa gharama ya Tsh.84,051,375.00, Ujenzi wa Barabara ya Ukwamani – Meshugi kwa gharama ya Tsh.205,334,275.00 pamoja na majengo manne ya Hospitali ya Wilaya yakiwemo majengo mawili ya Upasuaji kwa upande wa wanaume na wanawake, jengo la Dharura na nyumba moja ya Mtumishi.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.