• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro ataka kasi ya utendaji kazi sehemu ya viwanda, uwekezaji na biashara.

Posted on: September 4th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa akizungumza wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu na Wataalam wa idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ngazi ya Mkoa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Musa Ali Musa ameelekeza kuongeza kasi ya utendaji kazi katika sehemu ya uwekezaji na biashara kutokana na kuwa na mabadiliko makubwa ya teknolojia duniani kote ili kutoa huduma za uhakika na kuwezesha uchumi kukua Mkoani humo na Taifa kwa ujumla.

Alhaji Dkt. Mussa ameyasema hayo Leo Septemba 4, 2023 wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu na Wataalam wa idara ya viwanda, biashara na uwekezaji kutoka  Halmashauri za Mkoa wa Morogoro kinachofanyika siku mbili katika ukumbi wa mikutano wa Mbaraka Mwinshehe uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, kikiwa na lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji wataalam hao.

"...naamini kikao hiki kitaongeza ile chachu ya kutekeleza shughuli zake kwa kasi zaidi na mafunzo haya yakiwekwa vizuri kwa mifano halisi yatatunufaisha sisi wenyewe kwa kuwa na kasi katika utendaji pasipo kuwa na changamoto yoyote lakini pia yatawanufaisha watu wengine tuliopewa dhamana ya kuwahudumia..." Amesema Dkt. Mussa Ali Mussa.

Aidha, Dkt. Mussa ameelekeza wakuu katika kikao kazi hicho kutoa mafunzo kwa wataalam ili kuondoa changamoto zilizokuwa zikijitokeza hapo mwanzo zikiwemo kwenye Stakabadhi ghalani, Ushirika, SIDO na sehemu nyingine, hivyo amewataka wakuu na wataalam hao kuzingatia mafunzo hayo kwani ni Muhimu Kwa utendaji wenye tija kwa Taifa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa akiwa kwenye piacha ya pamoja na Wakuu wa Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji baada ya ufunguzi wa kikao hicho.

Aidha, Dkt. Musa ameelekeza katika kikao hicho cha kutoa mafunzo kwa wakuu na wataalamu hao  kuwapa elimu mahususi ya uelewa zaidi kwenye matumizi ya teknolojia hasa katika matumizi ya tarakilishi (computer), Vishkwambi (tablets) na simu janja (Smartphone) sehemu hizo na kuwa na wigo mpana wa utekelezaji wa majukumu ya vitengo hivyo.

Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Morogoro Bw. Kenneth Shemdoe akiwa kwenye kikao cha wataalam wa idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ngazi ya Mkoa.

Hapo awali Katibu Tawala msaidizi sehemu ya viwanda, biashara na uwekezaji Bi. Beatrice Njawa wakati akimkaribisha mgeni rasmi Dkt. Mussa amesema kikao hicho kinalenga kuwapitisha wataalam hao kwenye majukumu ya Msingi ya sehemu hiyo ili kuwajengea uwezo wa kufanya majukumu yao kwa ufanisi.

Katibu Tawala msaidizi sehemu ya viwanda, biashara na uwekezaji Bi. Beatrice Njawa akibainisha lengo la kikao kazi hicho cha wataalam wa idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Katika hatua nyingine Bi. Beatrice Njawa amemshukuru Katibu Tawala huyo Dkt. Mussa Ali Mussa kwa kukubali kuungana nao katika kikao hicho.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.