• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro ataka Ushirikiano kwa Madiwani, Watendaji na Wananchi.

Posted on: June 14th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba kuwa na ushirikiano baina ya  Wahe. Madiwani, Waatendaji na wananchi ili kuiletea maendeleo Halmashauri hiyo.

Bi. Mariam ametoa rai hiyo Juni, 12, mwaka huu katika kikao maalum cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo wakati wa kujadili ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali - CAG kilichofanyika Mlimba katika tarafa ya Mngeta Wilayani Kilombero.

Akizungumza katika kikao hicho, Bi. Mariam amesema ili kupiga hatua ya kimaendeleo kwa Halmashauri yeyote nchini ni budi kuwe na muunganiko wa pande hizo tatu na kama badala ya kuwa na misuguano ya mara kwa mara hivyo kuzorotehsha maendeleo.

“Muunganiko wa madiwani, watendaji na wananchi ndio njia bora ya kuleta maendeleo ya halmashuri ama wilaya husika, hivyo naomba muache maneno chapeni kazi ili mradi kila mmoja amuheshimu mwenzie amesema Bi. Mariam.

Aidha, amesema Halmashauri hiyo imekuwa mfano katika ukusanyaji wa mapato ya ndani na inafanya vizuri  katika mkoa wa Morogoro lakini ametahadharisha kuvunja makundi yaliyopo na kuimarisha ushirikiano baina ya pande hizo tatu ili Halmashauri hiyo iweza kuongeza zaidi ukusanyaji wa kimapato.

Katika hatua nyingine Katibu tawala huyo amewataka viongozi wa Halmashauri hiyo kubuni vyanzo vipya vya mapato badala ya kutegemea mapato ya zao la mpunga pekee huku akishauri kujikita katika kilimo cha zao la kakao kutokana na zao hilo kustawi vizuri katika maeneo mengi ya Halmashauri hiyo, kuwa na soko la uhakika na kakao yenye ubora zaidi.

Awali akitoa taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Nje Mkoa wa Morogoro Ndg. Mwabwanga Peter ameeleza namna kakao ya Mlimba ilivyotambulika nchi za ulaya kutokana na ubora wake hivyo ametoa wito kwa  madiwani kuwahamasisha wananchi kulima kwa wingi kutokana na upatikanaji wa soko hilo.

“Wakati nikiwa Ulaya nilipewa kakao ya kutoka hapa nyumbani na niliposoma kifungashio kiliandikwa imetoka Mbingu Mkoani Morogoro nikashangaa maana ni tamu sana na hata wao wanaipenda sana ”amesema Mwabwanga.

Kwa upande wa hoja za ukaguzi, Mwabwanga ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kujibu vizuri hoja za CAG katika kipindi cha mwaka 2018 – 2019 ambapo  hoja 19 kati ya 18 zilijibiwa kwa wakati na kubaki hoja moja ambayo ilitakiwa tamko la viongozi wa Mkoa huku kwa kipindi cha mwaka 2019 - 2020 hoja zilikuwa 24 kati ya hizo hoja 13.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Mhandisi Stephano Kaliwa amesema Halmashauri hiyo imepata hati inayoridhisha kwa miaka mitano mfululizo na kwa sasa wamebakiwa na hoja 10 ambazo zipo katika hatua ya utekelezaji.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.