• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO ATOA MIEZI MIWILI KUKAMILIKA KWA BARABARA YA ZEGE.

Posted on: June 11th, 2024


Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amemuagiza mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa Barabara ya zege ya Kinole - Tegetero - Lubwe kutoka kampuni ya (MacDavid Company limited) kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa barabara hiyo baada ya miezi miwili ili kusaidia Wananchi  wa maeneo husika kusafirisha mazao yao kutoka mashambani ili kuongeza kipato kwa wananchi wa eneo hilo.


Dkt. Mussa Ali Mussa ametoa agizo hilo Juni 11, 2024  wakati wa ziara yake kukagua miundombinu mbalimbali ikiwemo  barabara  hiyo ya zege katika Halmashauri ya Wilaya ya  Morogoro, ikiwa ni mwazo wa ziara yake ya kikazi ya siku tatu Mkoani humo.


"... sisi tunachukua hiyo miezi miwili kazi iwe imekamilika sasa nyie watu wawili mtoa kazi na mpewa kazi mkakae na mkajipange kuhakikisha huo muda kazi inakamilika.." amesema Dkt. mussa


Hata hivyo Dkt. Mussa amemuagiza mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa barabara hiyo kusogeza karibu vifaa vya ujenzi katika eneo la kazi ili kurahisisha upatikanaji wa haraka na kazi kwenda kwa kasi ili mradi huo uweze kukamilika kwa muda uliopangwa.


Kwa upande wake Bw. Enock Waitara Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro akisoma taarifa ya mradi amesema mradi huo wa barabara una urefu wa kilomita 1.0, unagharimu shilingi milioni mia 5.8 na ujenzi umefikia asilimia 25 huku ujenzi unatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 2 mwaka huu.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebeca Nsemwa  amesema kabla ya ujenzi wa barabara hiyo wananchi walikuwa wanapata shida katika kusafirisha mazao yao hivyo ameishukuru Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo ambapo itaenda kupunguza adha ya usafirishaji katika maeneo yao.

Katika hatua nyingine wananchi hawakuwa mbali kuishukuru Serikali yao kwa kuwaletea ujenzi wa barabara hiyo ya zege, akiwawakilisha wananchi wa maeneo hayo Bw. Rajabu Zahoro ameeleza changamoto zilizokuwepo mwazo kabla ya kuanza ujenzi huo kuwa  baadhi ya magari yalikuwa yanadondoka kwa kufeli kupanda mlima hivyo ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha zege itaenda kuwasaidia wakulima na wafanyabiashara kusafirisha mazao yao.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.