• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro atoa mwezi mmoja miradi ya SRWSS kukamilika

Posted on: September 4th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka watendaji na wasimamizi wa mradi wa usambazaji endelevu wa maji Vijijini na usafi wa mazingira wa ngazi zote za Halmashauri hadi za vijiji kukamilisha ujenzi ifikapo Oktoba, Mwaka huu.

Dkt. Mussa amesema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi ya ubaguzi wa mradi wa usambazaji endelevu wa maji Vijijini na usafi wa mazingira (SRWSS) katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ikiwa na lengo la kuinua kiwango cha usafi wa mazingira kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na jamii kwa ujumla.

Akifafanua zaidi, Katibu Tawala huyo wa Mkoa amesema mradi wa SRWSS unahusisha ujenzi wa vichomea taka, eneo la kunawia mikono pamoja na matundu ya vyoo kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa katika hali ya usafi kwenye vituo vya afya na zahanati, hivyo amewataka kukamilisha mradi huo mapema mwa mwezi oktoba mwaka huu.

"... mwezi wa kumi huo mliosema nisije nikasikia mara fedha zimetuishia, nataka miradi iishe mwanzoni wa oktoba..." amesema Dkt. Mussa Ali Mussa

Katibu Tawala huyo amesema vituo vingi vya zamani vimekuwa chakavu kutokana na kutokarabatiwa kwa sababu ya kusubiri fedha za Serikali kuu wakati fedha zinazopatikana katika vituo hivyo zinaweza kukarabati kwa kupaka rangi, kuweka sakafu na kubadilisha paa ili kuwa na mazingira bora.

Kwa sababu hiyo Dkt. Mussa amewataka madaktari  kujirekebisha na kuwa na maeneo nadhifu pamoja na usafi binafsi kwa 99% kutokana na kazi zao za kuhudumia wagonjwa.


Katika hatua nyingine, Dkt. Mussa Ali ameipongeza Kamati ya Kituo cha Afya cha Mlali ambao ndio wasimamizi wa mradi wa SRWSS kukamilisha mradi huo kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa na Serikali.


Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Dkt. Philipina Titus amesema kumekuwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za kimfumo hususan mfumo wa NeST unaohusika na manunuzi ambao mwanzo hawakupata mafunzo, mvua za El nino na ugonjwa wa kipindupindu ambazo zimesababisha mradi huo kuchelewa katika vituo vya afya na zahanati.


Naye, Afisa Afya wa Mkoa wa Morogoro Bi. Prisca Laurent Gallet amewasisitiza wasimamizi wa miradi hiyo kuitumia kwa kuitunza sambamba na kutunza nyaraka muhimu zikiwemo ramani na cheti cha ukamilishwaji wa mradi kwa ajili ya matumizi mengine.


Mradi wa SRWSS ulianza mwaka wa fedha wa 2022/2023 na kutekelezwa 2023/2024 katika Halmashauri zote za Mkoa huo ili kuwa na mazingira safi na salama tayari kwa kuhudumia wagonjwa.


Mwisho.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.