• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AUPONGEZA MFUKO WA TAO LA MASHARIKI.

Posted on: March 5th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameupongeza Mfuko wa Uhifadhi wa Milima ya Tao la Mashariki – EAMCEF, kwa kuhamasisha utunzaji wa mazingira na kuwapatia wananchi waishio karibu na maeneo ya hifadhi hiyo njia mbadala ya kujipatia kipato.

Dkt. Mussa ametoa pongezi hizo Machi 2, 2024 wakati wa ziara ya kutembelea baadhi ya maeneo yanayonufaika na ikiwemo kata ya Luhungo iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Baada ya kuwatembelea wanufaika wa ufadhili wa mfuko wa EAMCEF wa kata hiyo ya Luhungo, Dkt. Mussa Ali Mussa amebainisha mbele ya wananchi wa kata hiyo wanaonufaika na maradi huo kuwa lengo mahususi ni kupunguza umaskini miongoni mwao ili kuondoa uharibifu wa misitu hiyo. Miongoni mwa miradi iliyofadhiliwa na EAMCEF ni Pamoja na kuanzisha miradi ya kiuchumi ukiwemo ufugaji wa mbuzi wa maziwa, mradi wa uzalishaji uyoga na mradi wa matumizi ya majiko banifu.

Katibu Tawala huyo amesema miradi mingine ni mradi wa kilimo cha mazao ya viungo kama karafuu, Mdarasini, vanilla mchaichai na mbogamboga huku akiwataka wananchi wa maeneo ya hifadhi hiyo kuimarisha zaidi miradi hiyo ili kujipatia kipato na hatimae kupunguza uharibifu wa misitu.

“...ombi langu tufuge mbuzi kwa wingi, tuzalishe huo uyoga kwa wingi, ombi langu tupande michaichai kwa wingi, ombi langu tupande mikarafuu kwa wingi....” amesema Dkt. Mussa

Naye Afisa Maliasili Mkoa wa Morogoro Bw. Joseph Chuwa amesema Milima ya Tao la Mashariki ni safu za milima imepita katika mikoa Minne ya Morogoro, Kilimanjaro, Tanga na Iringa huku akibainisha kuwa miradi inayotekelezwa na Mfuko wa EAMCEF kwa Mkoa wa Morogoro unatekelezwa katika Halmashauri za tano za Mkoa huo ikiwemo Morogoro Manispaa, Mvomero, Halmashsuri ya Mji Ifakara, Mlimba na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

Bw. Chuwa ameongeza kuwa mito mikubwa ikiwemo mto Ruvu, Zigi, Wami, Ruaha na mto Pangani ambayo hutiririsha maji yao katika mikoa ya Iringa, Morogoro, Tanga, Pwani na Dar es Salaam huhu zaidi ya asilimia 25 ya wananchi wanaoishi karibu na milima ya Tao la mashariki wanategemea maji hayo kwa shughuli za mashambani na matumizi mengine.

Pia amesema, milima hiyo inachangia katika uzalishaji wa umeme ambapo kwa zaidi ya asilimia 50 ya umeme wote unaosambazwa hapa nchini Tanzania unatokana na maji huku akieleza kuwa mabwawa ya kuzalisha umeme ya Kidatu, Kihansi, Nyumba ya Mungu na Mwalimu Nyerere yote yanategemea maji kutoka misitu ya milima hii ya Tao la Mashariki

Kwa upande wao wanufaika wa miradi hiyo akiwemo Bi. Hanifa Salumu Mkazi wa Luhungo amewashukuru wafadhili wa mradi huo huku akibainisha kuwa alianza kufuga mbuzi wa maziwa mmoja hadi sasa ana mbuzi wanne hivyo mradi huo utamsaidia kupata kipato na kuacha kuharibu misitu iliyopo katika misitu ya milima hiyo kwa sababu ya kutafuta kuni.

Tao la Mashariki ni safu ya Milima iliyofunikwa na misitu yenye unyevu pamoja na mbuga katika nchi ya Tanzania na Kenya. Milima hiyo ina sifa ya kuhifadhi vyanzo vya maji ambayo hutumika kwa shughuli mbalimbali za kibinadamu ikiwemo matumizi ya majumbani, uzalishaji wa umeme na shughuli za kilimo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.