• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AWAFUNDA WATUMISHI WA UMMA

Posted on: June 24th, 2021

RAS morogoro awafunda watumishi wa umma.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja ametoa wito kwa Watumishi wa Umma Mkoani humo kujishughulisha na kilimo na Biashara ili kuboresha maisha yao na familia zao badala ya kutegemea mishahara ya kazi zao pekee.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro (RAS) Bi. Mariam Mtunguja wakati wa kikao cha kusikiliza na kupokea changamoto za watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Juni, 23 mwaka huu.

Bi. Mariam ametoa wito huo Juni 23 mwaka huu wakati wa kikao na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa alichokiitisha ili kufahamiana zaidi pamoja na kusikiliza kero walizo nazo watumishi hao kikao ambacho kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utumishi na Utawala Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Bw. Herman P. Tesha akisikiliza kwa makini maelekezo wakati wa kikao hicho.

RAS (aliyejivika kitambaa cheupe kichwani) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi yake mara baada ya kikao hicho. Ni picha inayoonesha kikao kimeamsha ari ya kazi kwa watumishi hao. Kazi iendelee.

Bi. Mtunguja amesema, kipato kinachotokana na mishahara yao pekee hakitasaidia kuboresha maisha yao kama watumishi hao hawatakuwa na njia nyingine ya kujikimu huku akiwashauri kujikita kwenye kilimo na biashara kazi ambazo amesema wanaweza kuzifanya baada ya masaa ya kazi za Ofisi.

“sisi tujishughulishe na kilimo, tujishughulishe na biashara na kwa bahati nzuri Mkoa wetu uko vizuri” amesema Mariam Mtunguja.

Watumishi wakionekana wana hamu ya kuendelea kusikia maneno yenye faraja kutoka kwa kiongozi wao - RAS 

Pamoja na kuwahamasisha watumishi hao kujikita katika kilimo na biashara amewatahadharisha wastaafu au watumishi wanakaribia kustaafu kutojiingiza kwenye biashara wasizozifahamu vema kwa kuwa wanaweza kutapeliwa kirahisi na kupoteza fedha zao.

“Msije mkajiingiza kwenye biashara ambazo hamzijui, ukiwa mstaafu usije ukajiingiza kwenye biashara usioijua watakuumiza, watu wamepigwa sana, afadhari hata kwenye kilimo..” amesisitiza Bi. Mtunguja.

kwa upande wao watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo akiwemo Leocardia Ramadhani na Pendo Daniel walieleza namna walivyompokea Katibu Tawala huyo na kubainisha kuwa amewatia moyo kwa kupokea changamoto zao na kuahidi kuzifanyia kazi. 

Aidha, wamempongeza kwa kuwajengea mazingira rafiki ya kuunda vikundi vya kusaidiana katika masuala ya kijamii yatakayosaidia kuondoa mifadhaiko wakiwa kazini na kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi.

Eric Olomi (Mchumi) kutoka Idara ya Mipango na Uratibu, akionekana kumkubali Boss wake Bi. Mariam Mtunguja kwa kile kinachotolewa nae wakati wa kikao hicho.

Naye Alhaji Hamisi Sengulo ambaye pia ni mtumishi katika Ofisi hiyo, yeye amekwenda mbali zaidi kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuteua Viongozi mahiri wa kumsaidia katika kazi ya kuwatumikia watanzania huku akiwataja Mkuu wa Mkoa wa Morogorogo Martine Shigela na Katibu Tawala wake Mariam Mtunguja kuwa kwa muda mfupi waliokaa, tayari wametoa maamuzi kadhaa ambayo yote yamelenga kupunguza kero za wananchi na kuwaletea maendeleo ya kweli.

Alhaji Hamis Sengulo akiwa katika kikao cha Katibu Tawala wa Mkoa huku akisikiliza kwa makini maelekezo yanayotolewa

 

watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakiwa katika kikao hicho, hapa wakitoa maoni, changamoto pamoja na mapendekezo yao kwa mtindo wa kuandika kwenye karatasi.

nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...KAZI IENDELEE

Imeandaliwa na Afisa Habari na Mahusiano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

(Picha zote na Andrew Tangazo Chimesela)

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.