• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro awasisitiza watumishi kufanya mazoezi, awataka kutumia mazingira mazuri yaliyopo

Posted on: August 4th, 2025



Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wametakiwa kutambua umuhimu wa kufanya mazoezi huku akiwataka kutumia vema mazingira mazuri ya Ofisi hiyo katika kufanya mazoezi kwa lengo la kuiweka timamu miili yao na kuepusha magonjwa madogomadogo yanayoweza kuepukika.

Kauli hiyo imetolewa Agosti 3, 2025 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro   Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi Alhaji Dkt. Mussa Ali  Mussa wakati akizindua rasmi klabu ya mazoezi ya Ofisi hiyo iliyofanyika eneo la maporomoko ya Maji ya CHOMA yaliyopo nje kidogo na Ofisi hiyo.


Amesema, Ofisi yake imefikia uamuzi wa kuanzisha “Club” hiyo inayojulikana kwa jina la “RAS MOROGORO JOGGING CLUB” ili kuimarisha Afya za watumishi wake na kutekeleza agizo la Serikali la kila Ofisi ya Umma iwe na program ya watumishi wake kufanya mazoezi ili kulinda afya za watumishi hao.

Aidha, amesema mazoezi hayo yatakuwa endelevu huku akibainisha kuwa yatakwenda sambamba na kutembelea maeneo ya utalii kama walivyotembelea maporomoko ya CHOMA ili kuyatangaza lakini pia kuyaboresha pale inapobidi kwa kushirikiana na mamlaka zinazohusika.

Amesema, Ofisi yake itakuwa tayari kushirikiana na Viongozi wa Sekta mbalimbali na kupeleka mahitaji muhimu kama UMeme, Maji, Barabara na huduma za Afya ili kuhakikisha Maisha ya wanaozunguka vivutio hivyo yanaboreka na kunyanyua Maisha yao Pamoja na kuongeza thamani ya maeneo hayo.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala huyo amesema  kuzinduliwa kwa klabu hiyo kunachocheo maandalizi ya kwenda kupata ushindi wa kishindo kwenye mashindano ya shirikisho la michezo ya wizara na idara za serikali (SHIMIWI) yanayotarajiwa kufanyika Jijini Mwanza kuanzia Septemba 1 hadi 16 mwaka huu.


Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Michezo Mkoa wa Morogoro Grace Njau amesema ili mazoezi ya watumishi kuwa endelevu imewekwa ratiba maalum ya siku tatu kwa wiki kuanzia saa 10:00 hadi saa 11:00 jioni watumishi wote wanaungana Pamoja kufanya mazoezi.

Naye Bw. Justine Mnyandwa kwa niaba ya watumishi wa Ofisi hiyo amesema kuwa kuna faida kubwa ya kufanya mazoezi hayo, amesema nje ya kuimarisha Afya za watumishi kwa kuepuka magonjwa yasiyoambukiza bado mazoezi hayo  yanadumisha Ushirikiano, Upendo na umoja miongoni mwa watumishi.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA VIJANA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

    August 12, 2025
  • WADAU WA MAONESHO YA NANENANE WAAGIZWA KUTEKELEZA WALIYOJIFUNZA

    July 12, 2025
  • RC CHALAMILA AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA MAONESHO YA NANENANE KUPATA ELIMU MPYA.

    August 06, 2025
  • RAS Morogoro awasisitiza watumishi kufanya mazoezi, awataka kutumia mazingira mazuri yaliyopo

    August 04, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.