• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro awataka ma DED kutoa Fedha kwa Wakaguzi wa Ndani.

Posted on: September 6th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro (RAS) Alhaji Dkt. Mussa Ali Mussa amewaagiza Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa huo kupeleka fedha kwenye vitengo vya Ukaguzi wa ndani Ili vitengo hivyo viweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe Dunstan Kyobya (wa tatu kulia waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa na Halmashauri pamoja na Wataalam wa idara ya Ukaguzi wa Ndani, wengine ni Katibu Tawala Wilaya ya Kilombero Bw. Abraham Mwaikwila, Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi Bi. Neema Dachi na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero  na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Morogoro CPA Peter Mwabwanga.

Dkt. Mussa Ali Mussa ametoa agizo hilo Septemba 5, 2023 wakati wa kufungua kikao kazi cha kawaida cha wakaguzi wa ndani Mkoani humo kilichofanyika Katika Mji wa Ifakara Wilayani Kilombero, amesema hayo kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Dunstan Kyobya.

CPA Peter Mwabwanga akielekeza Jambo wakati wa kikao kazi cha Wakaguzi wa Ndani kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi Bi. Neema Dachi.

Akisoma hotuba hiyo kwa niaba ya RAS, Mhe. Dustan kyobya amesema wakaguzi wa ndani katika Halmashauri wanazo changamoto nyingi, mojawapo na ufinyu wa bajeti, hata hivyo amewataka Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Mkoa huo kupeleka fedha kwenye vitengo hivyo kulingana na bajeti ya Halmashauri iliyopitishwa.

"...naomba kutoa rai kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro kuhakikisha; moja mnapeleka fedha Katika Vitengo vya Ukaguzi wa ndani kwa mujibu wa bajeti ya Halmashauri iliyopitishwa" amesema Dkt. Mussa Ali Mussa.

Aidha, amesema kwa kuwa Serikali inaendelea kuzifanyia kazi changamoto za Kitengo hicho ikiwemo idadi ya watumishi isiyo timilifu, uhaba wa vitendea kazi na ufinyu wa bajeti, bado amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kutoa ushirikiano wa kutosha kwa vitengo hivyo hususan kuwawezesha usafiri pale wanapohitaji kwenda kutekeleza majukumu yao ya kiofisi.

Katibu Tawala Msaidizi Sehem ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi Bi. Neema Dachi akiwa kwenye kikao kazi cha Wakaguzi wa Ndani.

Katika hatua nyingine Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka Wakaguzi wa ndani kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia miiko ya kazi zao lakini pia wajiamini huku akiwataka kutokuwa na kigugumizi cha kuwachukulia hatua za kisheria watumishi watakaobainika kufanya ubadhilifu wa fedha za Umma.

Sambamba na hayo amewataka kupunguza hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) zinazotokea Katika Halmashauri zao, kufanya ukaguzi wa ndani kila robo mwaka, kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye Halmashauri zao, kufanya kazi kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano - TEHAMA pamoja na kufanya kazi kwa ushirikiano baina yao na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya na Viongozi wengine wa ngazi ya Wilaya na Mkoa.

Kikao kazi hicho cha siku tatu kilikuwa na lengo la kukumbushana wajibu na majukumu ya Wakaguzi wa ndani huku Katibu Tawala wa Mkoa akitoa wito kwa wakaguzi wa ndani kufika Katika Ofisi yake mara wanapokuwa na changamoto zote.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.