• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AWATAKA WAALIMU KUWA WABUNIFU KUTUMIA VYAKULA VYA ASILI MASHULENI

Posted on: August 26th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka waalimu wa Shule za Sekondari na Msingi Mkoani humo kuwa wabunifu katika kuwapatia wanafunzi vyakula vya asili mashuleni ili wanafunzi hao waweze kujenga utimamu wa kimwili na kiakili kutokana na lishe inayopatikana kwenye vyakula hivyo.

Dkt. Mussa Ali Mussa amesema hayo Agosti 26, 2024 akiwa katika shule ya msingi Bamba iliyopo Kata ya Kiroka katika ziara yake yenye lengo la kutembelea shule mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kukagua vyakula vinavyoliwa mashuleni na wanafunzi ndani ya Halmashauri hiyo

Dkt Mussa amesema vyakula vya asili vinavyopatikana kwenye maeneo mengi ya Mkoa huo yakiwemo Mashelisheli, viazi, mihogo na ndizi vina lishe muhimu kwa watu wote hivyo vinapaswa kupikwa kwa namna tofauti ili kuwavutia wanafunzi kwa kuwa ndio vyakula vyao vya kila siku hivyo bila kuwaandalia vizuri hawatavutiwa na vyakula hivyo.

“… kuna vitu naomba mbadilike, kupunguza mzigo kwa wazazi ili hawa Watoto wote wapate kula, hilo tatizo limekuwepo ni kwa sababu walimu hamjataka kubadilika…” amesema Dkt. Mussa Aili Mussa

Aidha, Katibu Tawala huyo amesema vyakula hivyo vinapunguza gharama kwa wazazi kununua vyakula na kutoa fedha za ada ya wapishi ambapo hujikuta wazazi wachache wanachangia michango hiyo huku wengine wakitaka kutoa baadhi ya mazao ikiwa ni mbadala wa  michango hiyo.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mussa amewataka walimu wa shule hizo kulima mboga mboga na mazao ya biashara kama michikichi, mashelisheli na mikarafuu na kubainisha kuwa miche ya mikarafuu 40 inaweza kuleta faida ya shilingi 9 mil. ndani ya miaka minne hivyo shule husika kuweza kujiendesha yenyewe.

Kwa upande wake, Afisa lishe Mkoa wa Morogoro Bi. Salome Magembe amesema, vyakula vingi hususan vya mashuleni wanafunzi hawapati mlo kamili na kusababisha watoto kusumbuliwa na magonjwa.

Kwa sababu hiyo  Bi Salome amewasisitiza walimu kutumia mboga za majani za asili kwa wingi zikiwemo mchunga, mchicha pori, mnafu na majani ya kunde lengo ni kujenga afya ya watoto kwani mboga hizo hupatikana kwa urahisi.

Pia amesema walimu wanatakiwa kutumia matunda yaliyopo katika maeneo yao hususan maembe, machungwa na parachichi wakati wote wa chakula ili kutoa mlo kamili wenye lishe ya kutosheleza kwa Wanafunzi.

Naye, Mwalimu anayehusika na kuratibu upatikanaji wa chakula cha Shule ya Msingi ya Mtongozi Bw. Benard Swai amethibitisha kuwa katika shule hiyo wanafunzi wanatumia matunda ya mishelisheli na mboga mboga lengo ni kuweza wanafunzi  kuhimili darasani kwa kusikiliza na kuelewa kinachofundishwa.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.