• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AWATAKA WANANCHI KILOSA KUTUNZA MIUNDOMBINU YA BARABARA.

Posted on: June 13th, 2024


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka wananchi wilayani Kilosa  kutunza miundombinu ya barabara, madaraja na mitaro ya kupitishia maji ili iweze kutumika kwa vizazi vya sasa na vijavyo.


Dkt. Mussa ametoa wito huo Juni 13, 2024 wakati akikagua miundombinu ya madaraja ya Mazinyungu, Ilonga na Kobe yaliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro wakati akihitimisha  ziara yake ya siku tatu ya kukagua miundombinu mbalimbali ikiwemo ya barabara.


Dkt. Mussa amesema kuna umuhimu mkubwa wa wananchi wa maeneo hayo kutunza miundombinu hiyo ikiwemo kusafisha mitaro ya maji pindi inapochafuka ili kuepusha maji kutoka nje ya mitaro na kusababisha maafa kwa wananchi, huku akiwataka kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu ya barabara hususan alama za barabarani.


 "...ombi letu ni lilelile ili miundombinu hii ilete faida lazima itunzwe na isafishwe ikisafishwa inamaana itadumu..." amesema Dkt. Mussa 


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amesema  fedha  zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu yakiwemo madaraja ni Bilioni 36 na  zimefanikisha kukamilisha ujenzi wa madaraja matatu ambayo ni daraja la Mazinyungu, daraja la Kobe na Ilonga pia kupitia fedha za dharura zimesaidia kukamilisha ujenzi wa mitaro ya maji na kwenda kupunguza adha ya mafuriko Wilayani humo.


Aidha, Mhe. Shaka ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali wananchi wa Kilosa kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa madaraja na mitaro ya maji ambapo hapo awali walikuwa wanapata changamoto ya mafuriko kutokana na kutokuwepo kwa miundombinu hiyo.


Naye Diwani wa Kata ya Mvumi Ndg. Shabani Mabingo amesema kupitia ujenzi wa miundombinu hususan mitaro umeenda kuondoa adha ya mafuriko katika kata hiyo hivyo amemhakikishia Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro kuitunza kwa kushirikiana na wananchi ili iweze kuwa safi pindi mvua zinaponyesha maji yake yaweze kupita bila changamoto.


Nao wananchi wa Kilosa akiwemo Alfonce Dimoso mkazi wa Kijiji cha Mazese B wameishukuru Serikali kwa kukamilisha ujenzi wa madaraja hayo ambapo imeenda kuondoa changamoto ya usafiri na usafirishaji katika maeneo yao.


Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kilosa Mjini Irene Vedastus amesema hapo awali walikuwa wanatembea umbali mrefu kwenda shule kutokana na kutopitika kwa daraja la Mazinyungu hivyo kukamilika kwa daraja hilo kumewapunguzia umbali na kufika shuleni kwa wakati.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.