• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS Morogoro aipongeza TPA.

Posted on: November 24th, 2020

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo ameipongeza Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanazania – TPA kwa kuongeza ufanisi wa huduma za Bandari hapa Nchini na kuifanya TPA kuwa miongoni mwa mashirika ya Serikali yanayoongoza kwa kutoa gawio kwa Serikali.

Mhandisi Kalobelo ametoa pongezi hizo Novemba 23 mwaka huu akifungua michezo ya Bandari iliyoanza kufanyika katikaUwanja wa Jamhuri ulioko katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo na kushirikisha bandari zote za hapa nchini.

“Pia, napenda kutumia fursa hii kuipongeza Bodi ya TPA na Mkurunzi Mkuu wa TPA Mhandisi Deusdedit Kakoko pamoja na wafanyakazi wote kwa kuongeza ufanisi wa huduma za Bandari na kulifanya shirika letu kuwa moja ya mashirika ya Serikali yanayoongoza katika kutoa gawio kwa Serikali, hongereni sana” amepongeza Mhandisi Kalobelo.

Aidha, Mhandisi Kalobelo amesema, michezo hiyo kwa Mkoa wa Morogoro ni moja ya chachu katika Uchumi kwa kuwa uwepo wake unaongeza mzunguko wa fedha ndaniya Mkoa hususan kwa wafanyabiashara wa Morogoro wakiwemo wenye hoteli, nyumba za wageni na wasafirishaji.

Akiwa karibisha wanamichezo na viongozi wao Mhandisi Kalobelo amewataka kutembelea maeneo ya Utatlii yaliyopo katika Mkoa wa Morogoro ikiwemo mbuga ya wanyama ya Mikumi, Udzungwa, na hifadhi yaTaifa ya Mwalimu Nyerere ambayo sehemu kubwa ya hifadhi hiyo ipo katika Mkoa wa Morogoro.

Katika hatua nyingine Mhandisi Kalobelo amewataka wanamichezo kutoka katika Shirika hilo kufanya michezo hiyo kwa lengo la kutunza Afya na kushinda na kwa nidhamu lakini mara watakaporejea katika sehemu zao za kazi waende kufanya kazi kwa ufanisi, umakini na uadilifu wa hali ya juu.

Hata hivyo, amewakumbusha Wanamichezo hao kuwa ugonjwa wa UKIMWI bado upo hapa nchini hivyo amewataka kuendelea kuwa makini ndani ya mkusanyiko huo na kujikita katika michezo pekee lakini bila kufanya michezo na Afya zao.

Kwa upande wake Bi. Jayne Nyimbo kwa niaba ya Bodi ya Wakurugenzi wa TPA ameweka bayana kuwa Bandari ya Dar es Salaam na bandari nyingine zinaendelea kufanya kazi vizuri na ziko salama katika kuwahudumia wateja wake huku akiupongeza Mkoa wa Morogoro kwa kuwa na mchango mkubwa katika kusafirisha mizigo ya kutoka bandari ya Dar es Salaam kwenda nchi jirani.

Mkurugenzi Mkuu wa TPA Tanzania Mhandisi Deusdedit Kakoko ametaja malengo ya michezo hiyo kuwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu katika kazi zao, kujenga umoja miongoni mwao na kujenga Afya za wafanyakazi wao ili wakirudi katika mazingira ya kazi wafanye kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Michezo ya Bandari (Interports Games) kwa mwaka huu wa 2020 ni michezo ya 14 na inashirikisha Bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Bandar iJumuishi ya bandari zote za maji baridi yaani Bandari ya Maziwa na Shirika la Meli la Zanzibar. 

Kwa Mkoa wa Morogoro michezo hii imefanyika kwa mara ya tatu mfululizo huku ikihusisha michezo ya mpira wa miguu, kuvuata kamba kwa , kucheza bao na mingine mingi ambapo kwa mwaka jana Bandari ya Dar es Salaam ilibuka kidedea kama mshindi wa jumla kw amichezo yote.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.