• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC AANZA ZIARA YA KIKAZI,

Posted on: September 12th, 2022

RC Morogoro aanza ziara rasmi ya kikazi na kujitambulisha

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Abourbakar Mwassa ameanza rasmi ziara ya kujitambulisha kwa wananchi wa Mkoa huo katika Halmashauri zote tisa (9) za Mkoa huo lengo likiwa ni kuutambua vema Mkoa, kutambua changamoto zinazowakabili wananchi na kutambua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa alipofika katika mradi wa kituo cha kusukuma maji cha Kihonda

Fatma Mwassa ameanza ziara hiyo leo Septemba 12 katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ikiwa ni mara yake ya kwanza kufanya ziara ya aina hiyo tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo Agosti Mosi mwaka huu.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Ally Machela akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, alipotembelea miradi ya maendeleo

Akiwa katika Halmashauri hiyo Mkuu huyo wa Mkoa ametembelea miradi ya Maendeleo nane(8) ukiwemo mradi wa Shule ya Sekondari ya Boma yenye gorofa mbili Kituo cha Afya cha Tungi, Kituo cha Afya cha Lukobe, Shule ya Sekondari ya Lukobe, Hospitali ya Halamshauri ya Manispaa pamoja na Shule ya sekondari ya Mindu.

Miradi mingine aliyoitembelea ni ya Ujenzi wa Barabara ya Manzimbu inayojengwa na wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na ujenzi wa kituo kipya cha kusukuma maji eneo la Kihonda Mizani ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi 593 Mil.

Akiwa katika Mradi wa ujenzi wa Tanki la Maji Kihonda Fatma Mwassa amewataka wananchi wa Mkoa huo kutoharibu vyanzo vya maji kwa kuchungia mifugo katika maeneo hayo ya vyanzo vya maji na kutokukata miti karibu na maeneo hayo jambo ambalo amesema hatolivumilia kamwe.

Akisisitiza zaidi kuhusu utunzaji wa vyanzo vya maji Fatma Mwassa amewataka wanasiasa wakiwemo Waheshimiwa. Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa hiyo kuungana pamoja kukemea mwananchi yeyote anayeharibu vyanzo vya maji kwa kuwa maji ni uhai na kutumia fursa hiyo kuwataka waheshimiwa. Madiwani kuacha “siasa nyepesi”.

“Mimi niwaombe sana Waheshimiwa. Madiwani wangu, tusifanye siasa nyepesi nyepesi, kwenye suala la maji sheria lazima  ichukue mkondo wake vinginevyo hakutakuwa na sababu ya sisi kuwepo....”amesema Fatma Mwassa

Amesema upatikanaji wa Maji kwa Manispaa ya Morogoro ni 48% lakini serikali imeelekeza upatikana wa maji Mijini ni 98%, hii haimaanishi Serikali haijafanya kazi yake kuwapelekea wananchi maji la hasha, Serikali imeweka miundombinu ya maji ya kutosha takribani kila eneo changamoto ni uhaba wa maji yenyewe kunakotokana na uharibufu wa vyanzo vya maji kunakofanywa na wananchi wachache wasioitakia mema nchi hii.

Akitoa maelezo ya mradi huo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji Safi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA) Mhandisi Tamimu Katakwebe amemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa tanki hilo la maji linalojengwa  kwa shilingi 593.3 Mil. kwa fedha za Serikali amba[po kuna pampu mbili zenye uwezo wa kupandisha maji lita milioni 2 kwa saa 8 ambalo litanufaisha wakazi 120,000 wa kata za Kiegea, Mkundi na Mgulu wa Ndege.

Mkuu wa Mkoa fFatma Mwassa kesho Septemba 13 anaendelea na ziara katika Halmashauri hiyo ambapo anategemewa kuwa na Mkuatano na wananchim ili sikiliza kero zao na kuzitatua.

MWISHO

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.