• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Adam Malima aahidi kuifungua Wilaya ya Ulanga

Posted on: May 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema endapo changamoto kubwa zilizopo Wilayani Ulanga za miundombinu ya Barabara na upatikanaji wa uhakika wa Umeme ndani ya Wilaya hiyo zitaondolewa, Wilaya hiyo inakwenda kufunguka na kukua kiuchumi kwa na kwa mtu mmoja mmoja.


Mhe. Adamu Malima ametoa kauli hiyo Mei 25 mwaka huu wakati anaongea na watumishi wa Serikali wa Wilaya ya Ulanga pamoja na viongozi wa chama wakati wa ziara yake ya kujitambulisha ikiwa ni siku yake ya pili aliyoiaza Mei 24 mwaka huu Wilayani Gairo.


"naenda kuwa msemaji Mkuu wa Ulanga kwanza mkiondoa vikwazo mtaifungua Wilaya hii kupata bilioni 5 Kwa mwaka bila shida yoyote.. ubovu wa barabara za TANROAD gharama zote zitakazotumika kuleta lami Ulanga italipwa na maendeleo ya wananchi naona uzalishaji mkubwa sana..."

amesema Mhe. Adam Kighoma Malima.

Kwa upande mwingine, Mhe. Adam Malima amesema Mkoa wa Morogoro una ardhi ya kutosha kwa ajili ya kilimo hivyo amewataka wataalamu wa Wilaya hiyo kuweka mikakati ya kulinda ardhi hiyo ili kukidhi mahitaji ya wananchi wakizazi cha sasa na vizazi vijavyo Kwa miaka 50 ijayo.


Amesema, ni muhim kwa Viongozi wa Wilaya na Mkoa kuweka mikakati madhubuti ya kulinda rasilimali Ardhi iliyopo katika Wilaya ya Ulanga na Mkoa wa Morogoro kwa jumla kwa kuwa Ardhi ni rasilimali isiyohamishika lakini inayoongezeka thamani Kila inayoitwa Leo.


Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watendaji wote Mkoani humo  kuwa makini katika kutoa taarifa za kiutendaji na kuweka takwimu zote zinazohitajika, sahihi na zenye uhalisia kwani hizo ndizo zinazoongoza kupanga mipango ya maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi kujua  huduma zinazohitajika kwa kipindi Gani na na kwamba huduma hizo zielekezwe eneo gani.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameshauri watendaji ndani ya Mkoa huo kubadilika  kiutendaji na kwenda na Kasi iliyopo sasa kulingana na viongozi waliopo sasa.


Awali akitoa taarifa ya Wilaya ya Ulanga Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt. Julius Ningu alibainisha changamoto za Wilaya yake kuwa ni pamoja na  Migogoro ya wakulima na Wafugaji changamoto ambayo tayari Mkuu wa Mkoa ameitolea maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama kuifanyia kazi haraka na kumpa taarifa hatua waliyofikia.


Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa Adam Kighoma Ally Malima kesho Mei 26 inaendelea katika Wilaya ya Morogoro.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.