• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC aendelea na ziara Wilaya ya Morogoro, atatua migogoro ya wananchi.

Posted on: June 24th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amempa siku Saba mkuu wa idara ya ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Patrick Mwakilili kufanya tathmini upya umiliki wa ardhi baina ya Bw. Spilo mwenye Ardhi Eka 500, na Bw. Farid Ally ili kuona kiasi cha ardhi kikichobaki katika Kijiji cha Kiganila Kata ya Selembala katika Halmashauri hiyo.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akizungumza na wananchi wa Kata ya Selembala Kijiji cha Kiganila wakati wa ziara yake ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ya lukagua miradi ya maendeleo pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi.iliyofanyika Juni 23 mwaka huu.


Martine Shigela ametoa agizo hilo Juni 23 mwaka huu wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo pamoja na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi ambapo pamoja na mambo mengine ameitaka idara hiyo ya ardhi kuwasilisha Ofisini kwa Kiongozi huyo  ripoti ya tathmini hiyo kabla au ifikapo Julai mosi mwaka huu.



Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albart Msando akimkaribisha Mkuu wa Mkoa Martine Shigela ili kuzungumza na wananchi waakati wa ziara ya Mkuu huyo wa Mkoa Juni 23 mwaka huu.

Martine Shigela amesisitiza kwamba migogoro inayojitokeza baina ya wananchi na wawekezaji inatokana na sababu mbalimbali hukuakiwataka wawekezaji kuzingatia kiasi cha ardhi wanachopewa na wananchi na sio kujiongezea ardhi kwa kupora ardhi ya wananchi.

“Niagize idara ya ardhi kufanya tathmini upya kwa kumshirikisha Bw. Farid kuangalia umiliki wa ardhi hiyo kupitia nyaraka zake ili ardhi inayobakia waachiwe wananchi waendelee na utaratibu wao” ameagiza Shigela.

“Lazima tumiliki ardhi kulingana na uhalisia wa nyaraka tulizo nazo na ikifika tarehe mosi Julai naihitaji ripoti ya tathmini hiyo Ofisini kwangu” amesisitiza Shigela.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amekemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya wafugaji katika maeneo hayo vya kulishia mifugo kwenye mashamba ya wakulima ambapo jambo ambalo lilimkera na kulazimika kutoa agizo la kukamatwa kwa mfugaji mmoja aliyejulikana kwa jina la Mashaka ambaye mifugo yake inashutumiwa kuharibu shamba la mpunga la mkulima mmoja lenye zaidi ya hekari moja.






Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi ambaye ni Kamanda wa Jeshi hilo Mkoa wa Morogoro Fortunatus Musilimu akiongea na wananchi wa Kata ya Selembala wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Juni 23 mwaka huu.

Aidha, Martine Shigela ameitaka Wakala wa Maji Mjini na Vijijini - RUWASA kulipa mifuko 25 ya saruji  na DAWASA pia kulipa mifuko 120 ya saruji kwa kusababisha mifuko hiyo kuganda hivyo iletwe mifuko mipya kwa gharama za watendaji wa idara hizo ili shughuli za ukarabati wa visima 8 vya maji uweze kukamilika.




Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Kiganila Bw. Kondo Maulid amelalamikia baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi katika kituo kidogo Polisi tarafa ya Mvuha kutokuwajibika ipasavyo pindi wanapopewa taarifa za uharifu hususa kwa baadhi ya wafugaji kulishia mifugo yao mashamba ya wakulima.




Bw. Kondo ameeleza changamoto ya idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kutokushughulikia migogoro ya ardhi kijijini hapo kwa wakati hali inapelekea baadhi ya wananchi wa eneo hilo kukosa kufanya shughuli za uzalishaji.


Baadhi ya wananchi wa Kata ya Selembala Kijiji cha Kiganila wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela Juni 23 mwaka wakati ziara katika Kata hiyo.

 



MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.