• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC FATMA MWASSA AMSHUKURU RAIS DKT. SAMIA KWA BILIONI 200 ZA MAJI, AWATAKA WANANCHI KUTII SHERIA.

Posted on: December 21st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kutoa fedha zaidi ya Shilingi Bilioni 200 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji katika Mkoa huo.

Shukrani hizo zimetolewa Disemba 21 mwaka huu alipotembelea mradi wa ujenzi wa tanki la maji lililopo eneo la Kiegea katika Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Fatma Mwassa amesema Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani ametoa zaidi ya  shilingi Bilioni 200 ambapo fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi midogo  midogo ya maji ambayo itawanufaisha wakazi zaidi ya 120,000 wa Kihegea, Kihonda na Star City nashilingi Bilioni 185 kwa ajili ya uboreshaji wa bwawa la Mindu na ujenzi wa kituo cha kutibu  maji katika eneo la Mafiga katika Manispaa ya Morogoro.

Aidha, Mkuu huyo wa mkoa amesema Mkoa wa Morogoro unakabiliwa na kero kubwa tatu ambazo ni upatikanaji wa maji,  migogoro ya ardhi pamoja na miundombinu ya barabara hivyo Serikali imeweka juhudi kubwa katika kukabiliana na kero hizo ili kuzipunguza na kama ikiwezekana kuzimaliza kabisa.

Sambamba na hilo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro amewataka wananchi katika Mkoa huo kutii sheria na kutii taratibu za nchi zilizowekwa, pia amesema ili mtu aweze kujenga katika Mkoa huo  anatakiwa kuzingatia mambo matatu muhimu ambayo ni kuwa na Hati ya umiliki ya ardhi, mchoro ambao umeshibitishwa na Manispaa ya Morogoro pamoja na kibali cha ujenzi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Morogoro ( MORUWASA) Mhandisi Tamim Katakweba amesema ujenzi wa tanki hilo lenye ujazo wa lita milioni mbili na limegharimu kiasi cha shilingi Milioni 486 litasaidia kupunguza kero ya maji katika maeneo ya kihonda, kihegea lenye wakazi zaidi ya Laki mbili na Ishirini.

Aidha, Mhandisi Katakweba ameongeza kuwa mahitaji ya maji katika Mkoa huo ni Lita milioni 71 kwa siku lakini kwa sasa maji yanayopatikana ni lita 36 kwa siku ambayo ni sawa na asilimia 48 hivyo utekelezaji wa miradi hiyo katika Mkoa huo itapunguza kero ya upatikanaji wa maji.

Mkurugenzi huyo amesema Mradi wa uboreshaji wa bwawa la Mindu unatekelezwa kwa Bilioni 185 utahusisha uongezaji wa kina cha maji, ujenzi wa kituo cha kutibu maji katika eneo la Mafiga lenye ujazo wa lita milioni 54 pamoja na ujenzi wa matenki ya maji katika maeneo ya Lukobe.

sambamba na hilo Mkurugenzi huyo wa Moruwasa ameomba kupatiwa ardhi ili kuongeza ujenzi wa kituo cha kutibu  maji katika eneo la kihonda Mizani pamoja na ujenzi wa Ofisi kubwa ya Moruwasa.

Ziara hiyo ya Mhe. Fatma Mwassa ilianzia katika kituo cha kupokelea maji cha Mambogo, alitembelea bwawa la Mindu pamoja na mradi wa ujenzi wa tanki la maji katika eneo la Kihegea.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.