• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Kindamba asisitiza uzalishaji zaidi sekta ya kilimo, mifugo na Uvuvi

Posted on: August 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Waziri Kindamba ambaye pia alikuwa  Mgeni rasmi wa kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya Nanenane Kanda ya Mashariki, amewataka wakulima kuwa na uzalishaji wenye tija katika sekta ya kilimo, uvuvi na mifugo ili kukidhi mahitaji ya nchi na kupanua wigo wa biashara ndani na nje ya nchi.

Mhe. Kindamba amesema hayo Agosti 8, 2023 wakati wa kilele cha maadhimisho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yaliyofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Waziri Kindamba (wa pili kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Songoro Mnyonge, viongozi wengine katika picha hiyo ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge.

Mhe. Kindamba amesema kutokana na maonesho hayo anaamini kutakuwa na kilimo chenye tija kwa kujifunza teknolojia na mbinu za kisasa zinazoendana na mabadiliko ya tabia nchi kwani kwa kuongeza uzalishaji kupitia teknolojia mpya iliyotolewa Katika maadhimisho hayo itakuwa rahisi kupata masoko ya mazao hayo.

"... tutaweza kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo, uvuvi na ufugaji kwa ajili ya mahitajiya nchi yetu na ziada kwa ajili ya kuuza nje ya nchi Sina shaka na wakulima, wafugaji na wavuvi na wadau wote ambao tumepata fursa ya kutembelea Maonesho haya tumejifunza teknolojia na mbinu mpya ambazo tukizitumia vizuri zitasaidia kuongeza uzalishaji..." amesema Mhe. Waziri Kindamba.

Hapa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe Waziri Kindamba akisalimiana na mkulima wa zao la vanila kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

Aidha, Mhe. Kindamba amesisitiza kuwa teknolojia hizo za kilimo, ufugaji na uvuvi ziweze kuwafikia wakulima katika maeneo yao ili kuongeza ufanisi katika kazi na kutoa wito kwa sekta za umma na binafsi kushirikiana vyema na wakulima ili maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki kuendelea kuboreshwa kwa kuhimiza wadau kuleta teknolojia zitakazowapa elimu wakulima wa Kanda hiyo.

RC Kindamba akimkabidhi mkulima funguo ya trekta alilo nunua kutoka kampuni ya Agricom kwa ajili ya shughuli za kilimo.

Hata hivyo, Mhe. Kindamba amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ruzuku katika sekta ya kilimo na kupunguza bei za viwatilifu na mbolea, amesema Mhe. amefika hatua hiyo kwa kutambua umuhimu wa wakulima wenye hali ya chini ili kupata pembejeo hitajika hivyo kupata mazao ya kutosha.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima Kwa niaba ya  wanakamati wa Maonesho hayo Kanda ya Mashariki amewashukuru wadau mbalimbali wakiwemo Bodi ya sukari Kwa kujitoa kufanikisha Maonesho hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akipokea zawadi kutoka kwa viongozi wa Bodi ya sukari baada ya kutembelea banda hilo.

Mhe. Malima ameongeza kuwa wadau mbalimbali  ambao walitakiwa kuongeza nguvu wajipange ili Maonesho yajayo yawe Bora zaidi na kutaka kuwa na vipando vya kudumu vya Maonesho hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima katikati akiwa pamoja na Makatibu Tawala wa mikoa ya Morogoro na Tanga kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa, kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Bi. Pili Mnyema.

Maonesho hayo yamehitimishwa rasmi Leo Agosti 8, 2023 hata hivyo kutokana na wananchi kuendelea kuhitaji Elimu mbalinbali Katika viwanja hivyo maonesho yataendeleo kwa siku mbili zaidi hadi Agosti 10 mwaka huu.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.