• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AAGIZA MORUWASA, RUWASA KUTATUA KERO YA MAJI KWA WANANCHI

Posted on: January 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, ameiagiza Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Morogoro (MORUWASA) na Wakala wa Maji safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kukamilisha miradi ya maji inayotekelezwa ili kutatua kero ya maji kwa wananchi wa Halmashauri ya Manispaa na Mkoa huo.

Mhe. Adam Malima ametoa agizo hilo Januari 8, 2025, wakati wa kikao cha 42 cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Magadu uliopo Manispaa ya Morogoro.


Akifafanua zaidi, Mhe. Malima amesema suala la maji haliwezi kuvumilika hivyo hadi kufikia Januari 30 Mwaka huu Mamlaka hizo zimetakiwa kuandaa majibu ya namna ya kutatua kero hiyo ya maji.

… hadi tarehe 30 tunataka mje na majibu ya upatikanaji wa maji…” amesisitiza Mhe.Malima

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa huyo, amekemea tatizo la ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto unaotokea Mkoani humo na kutaka zitafutwe njia za kutatua tatizo hilo kwani amesema jamii inapaswa kulaani vitendo vya ukatili wa kijinsia, ikiwemo unyanyasaji wa wanawake, ubakaji, vitisho na ulawiti na matukio mengine yanayofanana na hayo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa, Dkt. Mussa Ali Mussa, amewataka viongozi wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri na Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji au Mitaa kushirikiana kuandaa mipango madhubuti ya kuondoa ukatili wa kijinsia kwenye maeneo yao.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Judith Nguli, amesema uwepo wa sheria nyepesi ndio sababu kubwa inayosababisha matukio ya ukatili Mkoani humo kuendelea kwa kasi.

Kwa sababu hiyo, Wajumbe wa kikao hicho kwa kauli moja wamekubaliana kupeleka kwenye mihimili ya kutunga sheria mapendekezo ya kubadilisha au kukaza sheria zilizopo  ili wale wanaobainika kujihusisha kufanya vitendo vya ukatili waadhibiwe kwa sheria hizo mpya.

Akiwasilisha mada hiyo Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Morogoro, ASP. Dkt. Mwanaidi Lwena, amesema kuwa ukatili wa kijinsia huathiri afya ya mwili na akili, na wakati mwingine kusababisha vifo, hivyo ameshauri kuwepo kwa mfumo unaoharakisha huduma za matibabu, ushauri nasaha, na ufuatiliaji wa kesi za waathirika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Joseph Masunga, watendaji kutekeleza kazi zao kwa weledi ili kukamilisha maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan hususan katika kusimamia miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao.

Akiwasilisha mada ya Sehemu ya Mipango na Uratibu Bw. Eric Olomi amesema kwa Mwaka wa fedha wa 2024/2025 Mkoa wa Morogoro umeidhinishiwa kutumia shilingi Bil. 4.8 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo, kati ya fedha hizo, fedha za ndani ni shilingi Bil. 3.4 na fedha za nje ni shilingi Bil. 1.4 ambapo zitatumika katika ujenzi wa miradi ya maendeleo na kukamilika kwa wakati.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.