• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima aagiza uongozi wa Kiwanda cha Mkulazi kutoa elimu kwa wakulima kuongeza uzalishaji.

Posted on: July 24th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ameuagiza uongozi wa Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi Mkoani humo kutoa Elimu kwa wakulima wa miwa kuongeza uzalishaji wa zao hilo ili kuwa na Mali ghafi ya kutosha kulisha Kiwanda hicho.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (wa tatu kushoto) akiwa pamoja na Viongozi mbalimbali wakitembelea maeneo mbalimbali ya kiwanda kipya cha sukari cha Mkulazi wakijionea maendeleo ya ujenzi wake.

Mhe. Adam Malima ametoa agizo hilo Julai 23 mwaka huu alipofanya ziara ya siku moja katika kiwanda kipya cha Sukari cha Mkulazi kilichopo Mbigiri Wilayani Kilosa ambacho kinamilikiwa na Mfuko wa Taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF) pamoja na Jeshi la Magereza.

Muonekano wa kiwanda kipya cha sukari cha Mkulazi kilichopo Mbigiri Wilayani Kilosa ambacho kitazalisha tani 50,000 kwa mwaka.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Kiwanda hicho ambacho kitazalisha tani 50,000 za sukari kwa mwaka kitapunguza uagizaji wa shehena za sukari kutoka nje ya nchi hivyo kitachangia upatikanaji wa ajira kwa watanzania.

Aidha, ameuagiza uongozi wa kiwanda hicho kuwaandaa wakulima ambao watazalisha miwa itakayo kidhi mahitaji ya kiwanda hicho.

“...sasa hawa wakulima wadogo huwa wanaandaliwa na ndivyo tulivyokubaliana sasa hivi na Bodi na watu wengine kuwa watengeneze mpango wa kuwaandaa wakulima ili waweze kuendana na mahitahi ya kiwanda...”. Amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amemtaka Mkandarasi anaye tekeleza mradi huo kukamilisha ujenzi wa kiwanda hicho kwa wakati ili kianze uzalishaji wake.

Katika hatua nyingine Mhe.  Malima ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kupitia Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kuanzisha Kiwanda cha sukari cha Mkulazi ambacho kitazalisha tani 50,000 za sukari kwa mwaka hapa nchini.

Nae, Bw. Filbert Mpozi Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025 Serikali haiagizi sukari kutoka nje, hivyo kiwanda hicho kipya kitatimiza lengo lake kutoagiza Sukari nje ya nchi.

Aidha, ameongeza kuwa kiwanda hicho kitaifanya Serikali kutotumia fedha nyingi za kigeni kuagiza sukari nje ya nchi lakini pia kiwanda hicho kitaongeza ajira kwa watanzania.

Hata hivyo, Bw. Filbert ameipongeza Serikali kupitia NSSF kwa uwekezaji huo ambao utaisaidia nchi kujitegemea kwenye bidhaa ya sukari.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Mkulazi Holding Company Dkt. Hildelitha Msita kwa niaba ya wajumbe wa Bodi hiyo amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa ziara yake na kuahidi kuyafanyia kazi maagizo aliyoyatoa ikiwemo kumsimamia mkandarasi ili aweze kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.