• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AELEZA HALI YA UWANJA WA JAMHURI.

Posted on: February 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewaeleza wadau wa mpira wa miguu na umma wa watanzania kwa ujumla kuwa hali ya uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri Mkoani humo uko vizuri na marekebisho ya kuelekea mechi ya timu ya Yanga Sports Club dhidi ya KMC  unaotarajiwa kuchezewa februari 17, 2024 katika uwanja huo yako vizuri.

Mhe. Malima amesema hayo Februari 10, 2024 baada ya kufanya ziara mahususi ya kuutembelea uwanja huo na kukagua maeneo ya ukarabati yanayoendelea kufanywa katika uwanja huo wa Jamhuri uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) baada ya kufanyika marekebisho ya sehemu ya kuchezea (pitch) limeridhishwa na ukarabati huo, huku jitihada za kukarabati vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji zikiendelea na kuhakikisha miundombinu mingine yote iliyobaki ukarabati wake unakamilika kwa wakati.

“….. Siku hizi mpira wa miguu unahusishwa na shughuli za kijamii na kiuchumi, hivyo sisi tunaiangalia hii Morogoro kama ni mji wa mpira na kwa maana hiyo starehe hiyo ya kuhakikisha  mpira unachezwa vizuri morogoro lazima ianzie hapa Jamhuri Stadium….” amesema Adam Malima.

Mhe. Malima amesema kuanzia mwezi Novemba, 2023 wamekuwa na mikakati ya kuuboresha uwanja huo ikiwemo kurudisha majani, kurudisha kijani, kuondoa sehemu za vipara pamoja na kusawazisha sehemu ya mashimo ya uwanja huo na kurudisha hali ya upatikanaji wa maji ya kumwagilia uwanja huo.

Katika hatua nyingine Mhe. Malima ameishukuru timu ya mpira wa miguu ya KMC kwa kuleta mechi hiyo uwanja wa Jamhuri - Mororgoro kama uwanja wao wa nyumbani huku akibainisha  kwamba mechi hizo zinasaidia kuingiza mapato kwa Halmashauri husika na kwamba halmashuri ya Manispaa ya Morogoro  itakusanya mapato kutokana na ukubwa wa mechi hiyo.

Kwa upande wake Meneja wa uwanja wa CCM Jamhuri Morogoro, John Simkoko amesema kuna maelekezo walipewa na TFF yakiwemo marekebisho ya sehemu ya kuchezea, kukarabati vyumba vya kubalishia nguo wachezaji pamoja na kurekebisha vyoo vya uwanja huo.

Hivyo, amemshukuru sana Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Kighoma Ali Malima pamoja na wadau wengine wa kabumbu mkoani humo kwa kuhakikisha ukarabati wa uwanja huo unakamilika kwa wakati na kuweza kufikia ubora unaotakiwa na shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania - TFF.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.