• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AIPONGEZA MTIBWA SUGAR AWATWIKA MZIGO VIONGOZI

Posted on: July 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ameipongeza timu ya Vijana chini ya miaka 20 ya Mtibwa Sugar ambayo imekuwa bingwa wa mashindano ya Vijana chini miaka 20 mara tano mfululizo, ikiwemo ubingwa wa mwaka huu, huku akiwataka viongozi wa timu hiyo kuweka mikakati madhubuti kuiendeleza timu hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akiwasalimia wachezaji wa timu ya Mtibwa Sugar ya vijana chini ya miaka 20 mara baada ya kuwasili Ofini hapo.

Mhe. Malima ametoa kauli hiyo Julai 7 mwaka huu wakati wa hafla fupi ya kuipongeza timu hiyo kwa kuwa bingwa mara tano mfululizo ikiwa ni pamoja na kubeba ubingwa wa msimu huu wa 2022/2023.

Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ambapo Mkuu wa Mkoa huo Adam Malima aliandaa chakula kwa ajiri ya kuwapongeza kwa ushindi huo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam Malima (wa tano kushoto waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wachezaji, viongozi wa timu ya Mtibwa Sugar pamoja na Viongozi wa Serikali kwenye hafla ya kuipongeza timu hiyo.

Mkuu wa Mkoa amesema kufanya vizuri kwa timu hiyo mara tano mfululizo ni jambo zuri, Vijana hao wakitunzwa vizuri wataleta mafanikio hadi kwenye timu ya Taifa, ili kufanikisha hilo amewataka viongozi wake kuwaendeleza Vijana hao ikiwa ni pamoja na kuwapandisha kuchezea timu kubwa ya Mtibwa Ili kupata uzoefu.

"...sasa Mimi nakuombeni hawa wachezaji ambao wametuthibitishia kuithamini Mtibwa na nyinyi muwathamini..." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Adam Malima amekubali ombi la viongozi wa timu hiyo la kuwa mlezi wa Mtibwa Sugar, hivyo ameahidi kufuatilia suala la viwanja ambavyo walikuwa wameahidiwa ili kuongeza maeneo ya kuendeleza vipaji vya vijana Mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akizungumza na viongozi, wachezaji na wadau wa sekta ya michezo wakati wa hafla ya kuipongeza timu ya Mtibwa Sugar.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa ameitakia mafanikio timu ya Wanawake ya Ifakara Queens ambayo inaenda kushiriki mashindano ya wanawake Mkoani Mwanza hivi karibuni.

Awali, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa timu hiyo Bw. Abel Magesa alimshukuru Mkuu wa Mkoa na kumpongeza kwa kuwa mdau wa michezo na kwamba  wanaamini sekta ya michezo Mkoani hapa sasa itafanya vizuri.

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa timu ya Mtibwa Sugar Bw. Abel Magesa akito shukrani kwa Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Bw. Abel amewasilisha ombi kwa Mkuu wa Mkoa la kuwa mlezi wa timu hiyo pamoja na kuwasaidia kupata viwanja walivyokuwa wameahidiwa na viongozi waliopita.

Nae, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa miguu Mkoa wa Morogoro kwa niaba ya viongozi wa Chama hicho wameahidi kutoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa ili kuhakikisha kuwa sekta ya michezo Mkoani humo inazidi kukua.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga akizungumza wakati wa hafla ya kuipongeza Mtibwa Sugar.

Kwa upande wake Athuman Makambo mfungaji bora wa mashindano hayo kwa mwaka huu amesema michezo ilikuwa migumu lakini kujituma kwao kuliweza kuwafanya kuwa mabingwa, hata hivyo, ameiomba Shirikisho la Soka hapa nchini (TFF) kuhakikisha kuwa mashindano yajayo yanaboreshwa.

Katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa ametoa zawadi ya jezi, mipira na fedha taslim Tsh. 1,000,000 ikiwa ni pongezi kwa timu hiyo kufanya vizuri.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Utawala na Rasilimali watu Bw. Herman Tesha (kulia) akiwa pamoja na Mhe. Rebeca Nsemwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro wakati  wa hafla ya kuipongeza Mtibwa Sugar.

Afisa Michezo Mkoa wa Morogoro Bi. Grace Njau (kushoto) akiwa na Afisa Elimu wa Mkoa huo Bi. Germana Mng'aho wakati wa hafla ya kuipongeza timu ya Mtibwa Sugar. 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.