• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima aitaka ASA, TARI kuzalisha mbegu bora za michikichi.

Posted on: June 12th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amezishauri Taasisi za Wakala wa mbegu za Kilimo - ASA na Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania – TARI Mkoani humo kuzalisha mbegu bora za michikichi ili kuwashawishi wananchi kujikita katika uzalishaji wa zao hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akiangalia miche ya michikichi kwenye moja ya kitalu kilichopo kwenye shamba la msimba Wilayani Kilosa.

Mhe. Malima amesema hayo Juni 11 mwaka huu alipotembelea Taasisi za Wakala wa mbegu za Kilimo - ASA na Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania – TARI Wilayani Kilosa ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo na kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali - CAG Mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema ili kuwahamasisha wanamorogoro kulima zao hillo la michikichi inatakiwa mbegu bora  hivyo watahamasika kulima zao hilo kwa tija.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akisaini kitabu cha wageni katika shule ya Msingi Mhovu mara baada ya kuwasili shuleni hapo kwa lengo la kukagua ujenzi wa shule hiyo.

“...kama tunataka watu wa morogoro wavutiwe na kilimo hiki cha michikichi, mbegu sahihi ni kila kitu...” amesema Mhe. Adam Malima.

Sambamba na hayo Mhe. Adam Malima amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri tano za Malinyi, Ulanga, Kilosa, Mlimba na Ifakara kuandaa maeneo kwa ajili ya vitalu vya michikichi ambayo itastawishwa na kuwagawia wananchi katika maeneo yao.

Hapa Mkuu wa Mkoa anakagua ujenzi wa shule shikizi ya Mhovu Wilayani Kilosa.

Katika hatua nyingine Mhe. Adam Malima amewataka wafugaji kuheshim jamii wanayoishi nayo kwa kutoingiza mifugo yao katika mashamba jamii hizo na kama watakaidi agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa mbegu za Kilimo - ASA Dkt. Sophia Kashenge amesema ASA imetekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa uzio wa Shamba la Msimba kwa gharama ya shilingi bilion 1.3, ukarabati wa gereji milioni 400, uzalishaji wa mbegu milion 300 na kufufua shamba la Msimba.

Mtendaji  Mkuu wa Wakala wa mbegu za kilimo - ASA Dkt. Sophia Kashenge akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa kuhusu shughuli wanazozifanya.

Sambamba na hilo Dkt. Sophia amesema katika shamba hilo wanalima mazao ya alizeti, mtama na choroko na kuahidi kuwa baada ya kukamilika kwa mifumo ya umwagiliaji watazalisha mazao mengi Zaidi.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.