• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AITAKA SUGECO KUTOA EKARI 200 KWA WANAKIJIJI.

Posted on: November 7th, 2024



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ameitaka taasisi ya Sokoine University Graduate Entrepreneurs Coorparative (SUGECO) ya Mkoani humo kuhakikisha wanawatafutia hekari 200 wananchi wa kijiji cha Lubungo zitakazowasaidia kulima na kuzalisha mazao ya bustani ili kuinua kipato chao na Mkoa kwa ujumla.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo Novemba 7, 2024 wakati akizindua mradi wa vijana wa kilimo cha mazao ya bustani kibiashara chini ya Programu ya Beyond Farming Collective (BFC) ambapo uzinduzi huo umefanyika katika kata ya Lubungo, Kijiji cha Lubongo Halmshauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.

Amesema, wananchi wa Kijiji cha Lubongo wametoa ardhi yao kwa ajili ya kutekeleza mradi huo ili waweze  kuwanufaisha hivyo ameitaka taasisi ya SUGECO kuhakikisha wanawasaidia wananchi hao kutenga hekari  200 ili waweze kugawana na kuzalisha mazao hayo ya hustani.

"... Lubungo wamekupeni shamba ili nyie na wao wanufaike nalo, kwa hiyo wao wamekupeni hekari 200 na wao wataweka ekari 200 pembeni na  lazima mzitafute .." Amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Aidha, Mhe. Malima amewasisitiza wafugaji wa Mkoa wa Morogoro kufuga kulingana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia ya sasa na kuacha ule ufugaji wa mifugo mingi isiyo na tija kwa mfugaji, hivyo amewahimiza wafugaji kuvuna mivugo yao na kufuga kisasa zaidi.

Katika hatua nyingine ameipongeze taasisi ya SUGECO na wadau mbalimbali kwa kushirikiana pamoja kutekeleza mradi huo kwa vitendo huku akiwataka wadau wote kuendelea kutekeleza mradi huo ili kuyafikia malengo ya kukifanya Kijiji cha Lubungo kuwa cha mfano  katika uzalishaji wa kisasa wa mazao ya bustani.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa SUGECO Mr. Revocatus Kimario amesema mradi huo unagharimu zaidi ya  shilishi Bilioni 1.13 ambapo unaenda kuwanufaisha vijana wasiopungua 1,820 huku akibainisha mazao yatakayozalishwa katika mashamba hayo kuwa ni matikiti maji, vitunguu na matango

Mr. Kimario ametoa wito kwa vijana wa Mkoa wa Morogoro hususan vijana wa kijiji cha Lubongo kuchangamkia fursa hiyo kwa kuwa miundombinu yote ya uzalishaji wa kisasa inaenda kukamilika hivyo ni wajibu wao kutumia mradi huo kuzalisha mazao ya bustan huku akiwahakikishia kuwepo kwa masoko ya uhakika wa mazao yatakayozalishwa.

Naye Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali Dkt. Rozalia Rwegasira amewataka wananchi wa Kijiji cha Lubungo kuupokea mradi huo kwa mikono miwili ambapo amesema utawasaidia kulima kilimo chenye tija, pia ameitaka taasisi ya SUGECO kuendelea kutoa elimu kwa wananchi wanaozunguka eneo la mradi kulima mazao yatakayowapa kipato.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.