• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AKAGUA RELI YA SGR MORO – KILOSA.

Posted on: July 4th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amefanya ziara ya kukagua ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kipande cha kutoka Morogoro hadi Kilosa kwa lengo la kuangalia hatua ya ujenzi iliyofikiwa pamoja na usalama wa treni hiyo inayotarajia kuanza safari zake katikati ya mwezi Julai 25, mwaka huu

Mhe. Malima amefanya ziara hiyo Julai 4, 2024 akiambatana na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ikiwa ni maandalizi ya utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutaka treni hiyo kuanza safari zake kwa kipande cha Morogoro – Dodoma ifikapo Julai 25, Mwaka huu.

Katika ziara hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema ameridhishwa na utendaji kazi unaoendelea wa kukamilisha ujenzi wa miundo mbinu ambayo ilikuwa haijakamilika ikiwemo ujenzi wa uzio (Fence) kwa ajili ya kuzuia wanyama pori kama tembo pamoja na mifugo huku akiagiza kazi hiyo ikamilike ifikapo tarehe 15 - 18 Julai.

“…sisi watu wa Morogoro tulipokea salamu, ya kwamba kuanzia tarehe 25 mwaka huu zitaanza safari za abiria kwenda Dodoma lakini kwa muda sasa, zaidi ya mwezi tuliweka angalizo kwa eneo hili…” amesema Mhe. Malima

Akikagua kituo cha treni cha Kilosa Mkuu huyo wa Mkoa amesema Kituo hicho cha treni cha Kilosa ni cha kimkakati kwa kuwa kitasaidia kukuza sekta ya Utalii Mkoani humo kwani amesema wageni wengi watakaotumia usafiri wa SGR wataweza kushuka Kilosa na kisha kutembelea Vivutio vilivyopo Mkoani humo vikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Nyerere, Mbuga ya Wanyama ya Mikumi, Hifadhi ya Milima ya Udzungwa,  na vivutio vingine vingi vilivyopo eneo hilo.

Katika hatua nyingine Mhe. Adam Kighoma Malima amekemea vikali tabia ya baadhi ya wananchi wanaojihusisha na wizi wa miundombinu ya Reli hiyo zikiwemo Nyaya za shaba huku akiwaonya kuwa watakaobainika watachukuliwa hatua kali za kisheria na mpaka sasa amesema tayari kuna baadhi ya watu wameshatiwa mbaroni wakihusishwa na wizi wa vifaa vya mradi huo.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kilosa Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amesema Kituo cha treni cha mwendokasi cha Kilosa kitafungua milango ya kiuchumi hususan katika sekta ya Utalii, Kilimo na Mifugo ambapo kumewekwa mkakati wa kushawishi watalii kutoka ndani na nje ya nchi kuanza kutembelea Vivutio na uwekezaji uliomo ndani ya Kilosa kupitia Reli ya SGR.


Hata hivyo, Mhe. Kabudi amebainisha kuwa Wilaya ya Kilosa ina utajiri wa kilimo cha mazao mbalimbali likiwemo zao la Vitunguu na mpunga hivyo kutokana na urahisi wa usafirishaji wa mazao hayo kutachochea uzalishaji wenye tija na kujenga Uchumi wa Wilaya, Mkoa na Taifa kwa jumla.  

  

Naye, Mkurugenzi wa Miundombinu wa Shirika la reli Tanzania Mhandisi Machibya Shiwa amesema zoezi la kuweka uzio limefikia 95% huku maeneo ya ushoroba wa Ngerengere na ushoroba uliopo katikati ya Kimambila na kimamba ni maeneo yanayojengwa uzio maalum wa kudhibiti wanyama wakiwemo tembo wanaotoka mbuga ya Mikumi.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.