• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AKEMEA MIGONGANO KWA WATUMISHI.

Posted on: June 24th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amekemea vikali  tabia ya baadhi ya watumishi kuendekeza tabia za majungu na migongano kazini kwa sababu zao binafsi na kusababisha kuzorota kwa shughuli za Serikali hususani ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa miradi ya maendeleo.

Mhe. Malima ametoa kauli hiyo Juni 24, 2024 wakati wa kikao cha Baraza maalum la wahe. Madiwani kwa ajili ya kupitia na kujadili hoja za Ukaguzi kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji Ifakara.

Mhe. Malima amesema kuna baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Ifakara wanaendekeza majungu na migongano hata kwa kiongozi wao ambaye ni Mkurugenzi hivyo kushindwa kutekeleza vema majukumu yao na kusababisha Halmashauri hiyo kuzidi kuzama huku akiwanyooshea kidole wahe. madiwani kushindwa kusimamia hali hiyo.

" .. Hatuwezi tukakaa kimya huku Ifakara inazama wao wanamagomvi nyie madiwani mnamagomvi hamsimamii miradi haiwezekani.." amesisitiza Adam Malima.

Aidha Kiongozi huyo amewataka watumishi wa Halmashauri hiyo na wahe. madiwani kujitathimini wao kama wapo kwa maslahi yao binafsi waache mara moja bali wafanye kazi kwa maslahi ya umma na kuwaletea wananchi maendeleo wanayohitaji.

" Kama wewe ni diwani nenda kajitathimini uko upande wa Diwani maendeleo au uko upande wa Diwani maslahi binafsi, kama wewe ni mtendaji kajitathimini, kama wewe ni mtendaji maendeleo au mtendaji maslahi binafsi..." amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Ifakara Mhe. Kassim Faya Nakapala ameonesha masikitiko yake ya kutokamilika kwa wakati ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri hiyo unaogharibu zaidi ya shilingi Bil. 7.4 ambapo ujenzi huo unatekelezwa na Tanzania Building Agency (TBA).

Akitoa salam kwenye kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa shughuli za Serikali Mkoani humo Dkt. Mussa Ali Musa ametumia fursa hiyo kuwataka wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa huo kupeleka Banki fedha zote za makusanyo katika Halmashauri zao kabla au ifikapo Juni 30. mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima kesho Juni 25 , 2024 ataendelea kuongoza kikao cha baraza la Madiwani  kama hicho cha kujadili hoja za Mdhibiti na  Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika HalmShauri ya Wilayani ya Kilosa.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.