• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima akemea ucheleweshaji wa ujenzi wa Shule Lipangalala, aagiza TAKUKURU kuchunguza.

Posted on: November 9th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amekemea tabia ya baadhi ya Viongozi Mkoani humo kutokamilisha miradi ya Maendeleo kwa sababu ya uwepo wa maelewano mabovu baina yao, hivyo kuwacheleweshea Wananchi Maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa na Wilaya alipotembelea ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Lipangalala.

RC Malima ametoa kauli hiyo ya karipio Novemba 8 mwaka huu wakati wa ziara yake alipotembelea ujenzi wa shule mpya ya Sekondari ya Lipangalala iliyopo katika Halmashauri ya Mji Ifakara Wilayani Kilombero Mkoani humo.

Akiongea na Viongozi wa Wilaya hiyo pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara amesema, kuendeleza ugomvi ambao unasababisha ucheleweshaji wa ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwemo shule ya mpya ya Sekondari ya Lipangalala ni kuwacheleweshea wananchi maendeleo na hivyo akawataka kuacha tabia hiyo la sivyo atachukua hatua.

Mafundi wakiendelea na ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Lipangalala.

“...kabla ya Rais Samia hajafanya maamuzi mimi nitakuwa nimeshawasimamisha ili yeye akafanye maamuzi mengine huko juu...” amesema  Mkuu wa Mkoa Adam Malima.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa huyo ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani humo kuchunguza chanzo cha ucheleweshaji wa ujenzi wa sekondari hiyo ambao ulitarajiwa kukamilika Oktoba 23, 2023 na kwa sasa bado upo katika hatua za kujenzi wa kuta.

Maagizo yake kwa vingozi hao kwa sasa ni kuwataka kuongeza kasi ya ujenzi huo kuendelea kujenga usiku na mchana ikibidi na kwamba anataka ukamilike kabla au ifikapo Disemba 31 mwaka huu.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro Ndg. Solomoni Kasaba amesema dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona wananchi wake wanapata huduma wakati wote huku akidai kuwa Chama hakitavumilia uzembe katika ukamilishaji wa miradi ya maendeleo kwa sababu ya mabishano ya viongozi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Ifakara Bi. Lena Nkaya ameeleza sababu za ucheleweshwaji wa ujenzi wa shule hiyo kuwa ni pamoja na mchakato wa manunuzi kuchukua muda mrefu na upatikanaji wa mkandarasi.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa shule hiyo mpya ya sekondari ya Lipangalala Msimamizi wa ujenzi huo Bw. David Chaula amesema mradi huo unagharimu shilingi milioni 528 ambapo inajumuisha ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa, jengo la utawala, chumba cha TEHAMA, Maktaba na vyumba 3 vya maabara.

Haya ni baadhi ya majengo katika shule mpya ya Sekondari ya Lipangalala inayoendelea na ujenzi.

Aidha, ameongeza kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa Oktoba 1 mwaka huu na ulitarajiwa kukamilika mwezi OKtoba 23,2023 ambapo Mkuu wa Mkoa ameagiza ukamilike ifikapo tarehe 31 Disemba, 2023.

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.