• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AONGELEA UTAJIRI WA MOROGORO, ASEMA UCHUMI WAKE UKO KATIKA SEKTA YA KILIMO.

Posted on: March 28th, 2024

RC Malima aongelea Utajiri wa Morogoro, asema Uchumi wake uko katika sekta ya Kilimo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Uchumi wa Mkoa  huo unapatikana katika sekta ya Kilimo kwa kuwa Mkoa huo una ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha na hali ya hewa inayofaa kwa kilimo cha mazao karibu yote muhimu yanayolimwa hapa nchini.

Mhe. Malima amesema hayo Machi 26, 2024 wakati wa kongamano la Chemba ya Wafanyabiashara wa Viwanda na kilimo (TCCIA) lililofanyika  hoteli ya Nashera, Manispaa ya Morogoro likishirikisha watu mbalimbali wakiwemo wakulima, wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda na taasisi za Kibenki.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Malima amesema, ili Wakazi wa Morogoro waweze kukuza Uchumi wao, wanawajibika kuanza kulima kisasa kwa kuwa kwa sasa suala sio kulima pekee, bali kulima kulingana na uhitaji wa soko.

“……. Lazima tufanye kilimo cha uzalishaji chenye tija kinachoendana na uhitaji wa Soko la nchi zingine hususan Nchi ya India…” Amesema Adam Malima.

Akizungumzia mahusiano baina ya Tanzania na India, mbele ya mwakilishi wa Balozi wa India Bw. Manoj Verma Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha umuhim wa Mkoa wa Morogoro kwenye mahusiano hayo kuwa yanatokana na utajiri wa Mkoa huo kwenye Sekta ya kilimo.

Amesema, kupitia mahusiano hayo, Mkoa wa Morogoro utanufaika kupitia Kilimo, kwa sababu India iko mbali kiteknolojia hivyo Tanzania wakiwemo wakazi wa Morogoro watapata ujuzi wa kilimo chenye tija kutoka India hususan kuzalisha mazao yao kwa wingi na kuboresha mazao hayo kulingana na masoko ya kimataifa.

Mhe. Malima amesema, mwaka 2024 Mkoa umejipanga kuzalisha miche milioni moja ya zao la mikarafuu na miche hiyo inatarajiwa kupandwa katika safu za milima ambayo imeharibiwa kutokana na shughuli za kibinadamu ikiwemo kukata mkaa, kuni pamoja na kilimo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Morogoro Mwadhine Mnyanza amesema lengo la kongamano hilo ni kuboresha mahusiano baina ya Nchi ya India na Serikali ya Tanzania hususan Mkoa wa Morogoro na Sekta binafsi ili kujenga uelewa wa Pamoja na kuweka mikakati inayotekelezeka husuan katika sekta ya kilimo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Morobatiki Group Dkt. Herriet James amesema kongamano hilo litaongeza uhusiano na litasaidia kupata malighafi ikiwemo upatikanaji wa rangi kwa bei nafuu na kwa urahisi hivyo litaongeza uzalishaji wa bidhaa ya Batiki.

+++++++++++++++             ++++++++++++ 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.