• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ARIDHISHWA NA UJENZI WA HOSPITALI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO

Posted on: June 21st, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema ameridhishwa na ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro baada ya kukamilisha sehemu ya ujenzi wa majengo hitajika na kutoa baadhi ya huduma ya Afya kwa wananchi wake.

Mhe. Malima ameyasema hayo Juni 20, 2023 wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa hospitali hiyo iliyopo takriban km 100 kutoka Mjini Morogoro.

Amesema, uwekezaji wa hospitali hiyo uliofanywa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unalenga kusaidia wakazi wa Halmashauri hiyo hivyo kupunguza umbali wa zaidi ya 100 km Kutoka Mvuha kwenda Morogoro mjini ambako walikuwa wanakwenda kupata matibabu.

"...ni mafanikio makubwa sana na kama hapa tulipo mimi mwenyewe nimefarijika sana, namshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wetu Kwa kuwekeza kwenye mambo kama haya..." Amesema Mhe. Adam  Malima.

Sambamba na Hilo, Mhe. Malima amesema ingawa hospitali hiyo haijakamilika kwa asilimia mia lakini imeendelea kutoa huduma ili kunusuru uhai wa Watanzania wa Halmashauri hiyo huku akiagiza kuweka kipaumbele katika kukamilisha majengo na utoaji wa huduma kwa akina mama, watoto na huduma ya maabara.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza watendaji wanaosimamia ujenzi huo kuongeza Kasi ya utekelezaji Kwani amesema uwiano uliopo wa majengo manne yanayotoa huduma kati ya majengo 14 hauridhishi.

Sambamba na agizo hilo amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuongeza idadi ya watumishi katika Hospitali hiyo zaidi ya 22 kuja kusaidiana na wengine 32 waliopo ili kupunguza majukumu kwa watumishi waliopo na kuleta tija kwa wagonjwa.

Awali, Mkuu huyo wa Mkoa  akiwa katika kituo cha afya cha Mikese ameagiza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Morogoro (RUWASA) kuchimbwa visima virefu vya maji ya uhakika ili kuondoa adha ya uhaba wa maji katika kituoni hicho cha Afya na kusaidia wananchi wa maeneo jirani.

Katika hatua nyingine akiwa katika kijiji cha Tambuu, Mhe. Adam Malima ameahidi kutoa miche ya zao la michikichi 5,000 ambayo wataigawa kwa wakazi wa Kijiji hicho kilichopo kata ya Lundi na kwamba kila kaya itapewa miche mitano ya kupanda kwenye mashamba yao lengo ni kuwaongezea wananchi zao hilo la biashara ili kuongeza kipato chao na kuongeza pato la Taifa

Naye Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Wilaya ya Morogoro Dkt. Kazimili Emanuel Subi, amesema hospital hiyo inawasaidia wakazi wa eneo hilo kutotembea umbali mrefu kufuata huduma ya Afya huku akibainisha uwepo wa madaktari bingwa watakao kuwa wanaletwa mara kwa mara hospitarini hapo ili kusogeza huduma za upasuaji karibu zaidi na wananchi.

Miongoni mwa wagonjwa akiwemo Bi. Fatuma Kibwana amewashukuru madaktari kwa kazi nzuri wanayoifanya na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea hospitari hiyo kubwa na yenye tija kwao.

Hospitali hiyo ya wilaya imeanza kutoa huduma za Afya tangu mwaka 2021 kukiwa na wastani wa wagonjwa 5 kwa siku na sasa inapata wagonjwa zaidi ya 30 kwa siku ikitoa huduma  ya wagonjwa ya kulaza wagonjwa, maabara, mionzi, x-ray pamoja na ultrasound.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.