• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ASISITIZA UTULIVU, ORODHA YA WAATHIRIKA KUPEWA KIPAUMBELE

Posted on: April 26th, 2024

Siku chache baada ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kutoa agizo la kutoa pole na misaada ya mahitaji muhimu kwa waathirika wa Halmashauri ya Mlimba kupitia usafiri wa anga (Helicopter ) kutokana na miundombinu ya Halmashauri hiyo ikiwemo Barabara kuharibiwa na kusababisha kutokufikika katika maeneo ya kata ya Masagati na Utengule limeanza kutekelezeka.

Agizo hilo limeanza kutekelezwa aprili 26, 2024 ambapo likisimamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya maafa Mkoani humo ikiwa usafiri huo unatokea Ifakara Mji kupeleka misaada Halmashauri ya Mlimba Wilayani Kilombero.

"... na mkumbuke Waziri Mkuu alisema nini alisema hapa kuna orodha ya wahanga sasa ndio wanaokusudiwa kwanza jamani kuna watu wamepoteza kila kitu kwanzia nyumba, chakula na shamba hao ndio wapewe kipaumbele..." amesema Malima

Aidha, Mhe. Malima amesema mahitaji hayo ni zaidi ya tani 6 ambayo yametoka serikali kuu na kwa wadau mbalimbali wakiwemo wa sekta binafsi na sekta za umma na kuungwa mkono na Wabunge wa Wilaya hiyo katika kufanikisha wananchi wanasaidiwa kulingana na uhitaji wakiwa na lengo la kutoa pole na kuwafariji waathirika wa janga la mafuriko Wilayani humo.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa mahitaji ya Mkoa ni mengi kulingana na mafuriko yanayoharibu miradi ya maendeleo na makazi ya wananchi pamoja na mazao yaliyo mashambani, hivyo wananchi wa Wilaya za Malinyi na Ulanga serikali inaendelea na mchakato wa kuwafikia ili kutoa msaada.

Kwa upande wake, Kamishina msaidizi mwandamizi wa Jeshi la zimamoto na uokoaji ambaye ni mratibu wa maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Ivan Alfred Ombela amesema kuwa mchakato huo wa upelekaji wa misaada ya chakula mbalimbali ikiwemo mchele, maharage, sukari, na unga katika Halmashauri ya Mlimba ambapo kuna jumla ya waathirika 1900 kwenye kata mbili za Masagati na Utengule.

Pia, ameongeza kuwa katika kata hizo Kamati za maafa za kata zinahakikisha waathirika wote wa mafuriko kupata mahitaji hayo kutokana na utaratibu uliopangwa.

Naye, Bi. Rainoda Peter Kilangavana Mkazi wa Masagati ameishukuru serikali kwa kutoa misaada mbalimbali katika kata hiyo na kuiomba serikali sikivu kutatua changamoto ya Kituo cha Afya baada miundombinu kuharibiwa hivyo kina Mama wajawazito kushindwa kupata huduma kwenda Kituo cha Afya cha Halmashauri ya Mlimba.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.