• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima ataka ushirikishwaji wa uhamasishaji chanjo.

Posted on: February 13th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka waratibu wa chanjo na magonjwa yasiyopewa kipaumbele kwenye jamii Mkoani humo, kushirikisha wadau mbalimbali hususan viongozi wa dini kwenye zoezi la uhamasishaji wa chanjo ya Surua Lubera na utoaji dawa kwa magonjwa yasiyopewa kipaumbele kama vile Usubi, Matende, Mabusha na Kichocho.

Mhe. Malima ameyasema hayo Februari 12, 2024 wakati wa kikao cha Afya ya Msingi kilicholenga uzinduzi wa kampeni ya Chanjo ya Surua Lubela na Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Mkoani humo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Viongozi hao wa Dini wanaushawishi mkubwa kwenye jamii  hivyo kupitia nyumba za ibada walizopo watahamasisha wananchi wengi kuitikia zoezi hilo la utoaji wa chanjo ya Surua na dawa za magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele   ambalo linatarajiwa kuanza Februari 15 hadi 18, 2024 Mkoani humo.

"...kwa sababu kwenye mambo haya ninyi hamuwezi kupeleka meseji kwa uwezo wanaopeleka... wao ijumaa, jumamosi na jumapili wanapata watu wengi kuliko utakaopata wewe..." amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Malima amewataka wananchi kuacha kung'ang'ania mila, desturi na imani potofu hususan kwenye suala la chanjo kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa amewataka waratibu hao kufikisha ujumbe kwa jamii kwa kutumia picha halisi ya madhara ya magonjwa hususan yale yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwenye jamii yakiwemo Matende, Mabusha, Usubi, Trakoma, Kichocho na Minyoo.

Naye, Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Morogoro Dkt. Masumbuko Igembya amesema kampeni ya utoaji chanjo ya Surua Lubela Mkoani humo itafanyika ndani ya siku nne kuanzia Februari 15 hadi 18, 2024  na kuwafikia watoto 368555 wa Mkoa huo wenye umri kati ya miezi 9 hadi 59 huku akiwataka wazazi kuhakikisha kuwa watoto hao wanapata chanjo hiyo.

Kwa upande wake Mratibu wa Magonjwa  yaliyokuwa hayapewi kipaumbele  Mkoa wa Morogoro Dkt. Debora Kabudi amesema hapa nchini kuna magonjwa 5  ambayo yaliyokuwa hayapewi kipaumbele magonjwa hayo ni pamoja na Usubi, Kichocho, Matende, Minyoo ya tumbo na Mabusha.

Amesema, Mkoani Morogoro kuna ugonjwa wa Usubi ambao umeathiri  Halmashauri 8 za Mkoa huo pia amebainisha kuwa Mkoa umeanzisha kampeni ya kutokomeza magonjwa hayo ikiwa ni pamoja na kutoa dawa za usubi, Minyoo ya tumbo na kichocho kwa wanafunzi wa shule za msingi ambapo zoezi linatarajiwa kuanza Februari 15, 2024.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.