• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

Posted on: May 15th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amevitaka vyama vya ushirika vinavyojishughulisha na mifugo kufuga kisasa ili kuwa na mifugo bora itakayo kuwa na uzalishaji wenye tija kwao na taifa.


Mhe. Malima amesema hayo Mei 15, Mwaka huu wakati akifungua Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Morogoro lililofanyika ukumbi wa mikutano wa Mbaraka Mwinshehe uliopo Manispaa ya Morogoro.


Mhe. Malima amesema faida ya kufuga kisasa na kuwa na mifugo bora kutaongeza pato la Serikali kwani wafugaji wataweza kulipa kodi kutokana na mifugo yao, kuendesha maisha yao hivyo kupunguza pia migogoro inayotajwa kuwa ni ya wakulima na wafugaji.


Kwa sababu hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Maafisa Ushirika na Maafisa Mifugo wa Wilaya za Mvomero na Kilosa kuanzisha vyama vya Ushirika vya wafugaji na kuvipatia elimu ya kufuga mifugo yenye tija ili kuondokana na migogoro katika Wilaya zao.


Katika hatua nyingine, Mhe. Adam Malima amewakumbusha wananchi wa Mkoa huo kwenda kuhakiki taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili itakayoanza Mei 16 hadi 22, 2025 ili kujipatia vigezo vya kupata fursa ya kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu.


Naye, Mrajis Msaidizi wa uhamasishaji na uratibu TCDC Bw. Ibrahim Kadudu amesema vyama vya ushirika vinapaswa kuwekeza na kutoa fursa kwa vijana, wanawake na  watu wenye ulemavu ikiwa ni njia ya kusaidia kuimarisha jamii nzima.


Kwa upande wao wafugaji akiwemo Bi. Pendo Ndemo wa chama cha ushirika cha  Namayana kutoka Mvomero wamekiri kuwa bado wanafuga bila kuzingatia utaalamu hali inayopelekea kupata faida kidogo inayotokana na mifugo hiyo hivyo wamemuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia wataalam wa kutoa elimu kuhusu ufugaji wenye tija.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.

    May 14, 2025
  • WANAFUNZI 214 WA KIDATO CHA KWANZA SEKONDARI ZA MONGOLA, MGETA WAPEWA MICHE 2140 YA MIKARAFUU

    May 13, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.