• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATAKA WANANCHI KUPIMA AFYA WAKATI WA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA

Posted on: April 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushiriki kupima Afya zao wakati wa Kambi Maalum ya Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia Suluhu Hassani (Outreach Services) ili kukabiliana na magonjwa waliyonayo au yale ambayo wanayo bila ya wao kujua.

Mhe. Malima ametoa wito huo Aprili 29, Mwaka huu wakati akiongea na waandishi wa habari akitoa taarifa ya kambi hiyo itakayofanyika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuanzia Mei 6 hadi 10 2024.


Mkuu wa Mkoa Adam Kighoma Malima amesema, kambi hiyo maalum inayojulikana kama ni ya kanda ya kati inayojumuisha Mikoa ya Dodoma, Iringa, Singida, Pwani na wenyeji Morogoro itapokea wananchi wote wanaotaka kupata huduma hiyo maalum na yenye gharama nafuu kwa wananchi kutoka Mikoa hiyo iliyotajwa hapo juu.


Aidha, amesema, Kambi hiyo inakadiriwa kutoa huduma za afya kwa wagonjwa 200 na kufanya upasuaji kwa wagonjwa 100 kwa siku watakazokuwepo kambini ambapo huduma zote za kumuona daktari zitatolewa kwa Tsh. 5000 pekee, hivyo wananchi wenye matatizo mbalimbali na wanaotaka kujua afya zao na kutaka ushauri watatakiwa kufika kambini hapo.

Sambamba na hilo, Mhe. Adam Malima amewataka Wakuu wa Wilaya zote na Wakurugenzi kuhamasisha wananchi katika maeneo yao na kutafuta namna bora ya wagonjwa kuweza kujisajili na kufika katika kambi hiyo ili kupata huduma hiyo.

Hata hivyo amebainisha njia zitakazotumika katika kujisajiri mapema kabla ya siku au tarehe za kupata huduma hiyo ikiwemo wananchi kwenda kuwaona Wakuu wa Wilaya zao, kuwaona Wabunge wao na Wakurugenzi wa Halmashauri zao na hata kupiga simu ambazo ni 068343 5656 na 0783658931.


Awali, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Kusirye Ukio amesema kuwa Kambi hiyo itakuwa na Madaktari 54 ambao wanatoka katika Mikoa minne (4) ikiwa na lengo la kufikisha huduma kwa wananchi  sambamba na kutoa ujuzi kwa madaktari waliokaribu na eneo la tukio, hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto nyingi za Afya kwa wananchi wa Mikoa ya Pwani, Morogoro, Iringa, Singida na Dodoma.


Naye, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Daniel Nkungu akijibu maswali ya waandishi wa habari alisema kuwa changamoto zote za kiafya zinazowakumba wagonjwa zikiwemo wanawake wanaosumbuliwa na uzazi, watoto, na kusisitiza kuwa WANANCHI WANAOHISI WAKO SAWA KIAFYA HUSUSANI WANAWAKE wafike kufanya vipimo vya afya (check up ) ili kupata ushauri na matibabu, kwan mara nyingi wznafika kufanya vipimo tayari wanakuwa wamechelewa na ugonjwa kuwa vigumu kutibika.


Katika kuhakikisha serikali inasogeza huduma za afya karibu na wananchi, Wizara ya afya kushirikiana na hospitali za rufaa za Mikoa ya Morogoro, Dodoma, Iringa, Singida na Pwani (Tumbi) itahusika kutoa huduma ya Afya kwa wananchi kupitia kambi maalum iliyoelezwa hapo juu.

Magonjwa yaliyopewa kipaumbele kutibu ni pamoja na magonjwa ya watoto, wanawake na uzazi, masikio, pua na koo, upumuaji, magonjwa ya ndani (Moyo, figo, kisukari na shinikizo la damu), mfumo wa mkojo, mifupa, ngozi, macho, kinywa na meno, Afya ya akili, utengamano, mfumo wa chakula na huduma ya usingizi tiba na ganzi.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.